Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini, Mhandisi Ngosi Mwihava (katikati) akimkabidhi cheti cha kuhitimu mafunzo ya lugha ya Kireno Zahoro Athmani mmoja kati ya wanafunzi 15, waliohitimu mafunzo hayo, ambapo 7 kati yao tayari wamepata ufadhili wa masomo ya Shahada za Uzamili na Uzamivu katika fani za mafuta na gesi nchini Brazili. Kulia ni Balozi wa Brazili nchini, Fransisco Carlos Luiz, akimpongeza mwanafunzi huyo.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini Mhandisi Ngosi Mwihava, akiongea na wanafunzi waliopata waliohitimu mafunzo katika lugha ya Kireno ambapo saba kati ya 15 tayari wamepata ufadhili wa kujiunga na vyuo vya mafuta na gesi nchini Brazili, Kushoto ni balozi wa Brazili nchini Fransisco Carlos Luiz (kushoto), wengine katika picha ni baadhi ya watumishi kutoka Kampuni ya kuchimba gesi ya PETRO Bras, Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), na Wizara ya Nishati na Madini.
Balozi wa Brazili nchini Fransisco Carlos Luiz (wa pili kulia) akiongea jambo na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini Mhandisi Ngosi Mwihava (kushoto) baada ya kuwakabidhi vyeti wanafunzi 15 waliohitimu mafunzo ya lugha ya kireno kabla ya kujiunga na masomo ya Shahada za Uzamili na Uzamivu katika fani ya mafuta na gesi , saba kati yao.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini Mhandisi Ngosi Mwihava (wa nne kulia) na Balozi wa Brazili nchini Fransisco Carlos Luiz (wa tatu kulia) katika picha ya pamoja na Wanafunzi 15 walihitimu mafunzo ya lugha ya Kireno. Wanafunzi 7 kati yao tayari wamepata ufadhili wa kusoma masuala ya mafuta na gesi katika ngazi za Shahada ya Uzamili na Uzamivu nchini Brazili mwezi Machi mwakani.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...