Watumiaji wa simu za mkononi wameendelea kukua  kadri siku zinavyo endelea na kumekua na maswali mengi jinsi gani mtu anaweza kubaki salama atumiapo simu za mkononi.
Hapa nitaangazia uhalifu mtandao unao ambatana na simu za mikononi na njia za matumizi salama ya simu za mkononi. Nianze kuangazia uhalifu unaoweza kusababishwa na simu za mkononi.

Swapping: Huu ni uhalifu mtandao unao kua kwa kasi hivi sasa maeneo mbali mbali unaotoa fursa kwa mhalifu mtandao kuwa na matumizi ya simu ya mtu bila ya mwenye simu kujua. Mara nyingi wahalifu mtandao wana lenga kuiba pesa au kuwasiliana na watu wa karibu wa mtumiaji halisi wa simu ya mkononi kwa sababu tofauti tofauti.


Hii inatokea pale mhalifu mtandao anapo kua amepata namba yako ya simu na kusoma  ratiba yako hasa muda gani unakua hauna matumizi makubwa na simu – Baada ya kujua hivyo kupitia programu zilizopo sasa zina mpa fursa kukutoa hewani na kuanza kuitumia namba yako ya simu  ambapo anaweza kufanya mengi baada ya kua na umiliki huo ikiwa ni pamoja na kutoa au kuhamisha pesa zako na pia kuitumia vibaya simu yako. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...