Pichani ni Mkurugenzi Mkuu wa TFDA Bw. Hiiti Sillo akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) katika mkutano na waandishi wa habari katika kueleza maamuzi ya TFDA kufuta usajili na kubadili matumizi ya baadhi ya dawa nchini. Mkutano huo ulifanyika katika ukumbi wa TFDA Makao Mkuu

 Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) imezifutia Usajili wa Dawa tano  za Binadamu kutokana na kuwepo makosa mbalimbali.         Hayo yameelewa leo jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi mkuu   TFDA Bwana Hiiti B.Sillo  Wakati wa Mkutano na Waandishi wa Habari ambapo alisema Mamlaka hiyo katika kupitia mifumo ya ufuatiliaji  wa usalama na ubora wa dawa nchini wamebaini uwepo wa dawa duni kwenye soko zenye madhara na zisizofaa kwa matumizi ya Binadamu.

         Mkurugenzi Mkuu alieleza kuwa TFDA imefikia hatua ya kufuta   usajili wa aina tano za dawa za binadamu ambazo ni Dawa ya kutibu “Fungus” ya vidonge na kapsuli aina ya ketocanazole kwa sababu dawa hiyo inasababisha madhara hatarishi katika Ini kwa watumiaji.

          Dawa nyingine ni ya kutibu malaria ikiwa katika mfumo wa maji na vidonge aina ya Amodiaquine inapotumika yenyewe na sababu ya kufutia usajili na kuzuia kuingia nchini ni kutokana na mabadiliko ya mwongozo wa kisera wa kupima na kutibu malaria wa mwaka 2013 uliotolewa na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, na kwamba ikitumika peke yake inaleta usugu wa vimelea vya malaria.

         Bw. Sillo aliitaja dawa nyingine  ambayo ni hatari kwa matumizi ya binadamu ni Dawa ya  kutibu mafua na kikohozi ya Maji,Vidonge na Kapsuli zenye kiambato hai aina ya Phenylpropanol amine ambacho anasema kinaleta madhara hatarishi kwa binadamu kama vile kiharusi (Hemorrhagic sroke).

           Mbali na hizo Dawa zengine ni Dawa ya kuua bacteria ya Sindano aina ya Chloramphenicol Sodiam Succinate inayotengenezwa nchini India pamoja na dawa ya kuua Bakteria ya Maji na kapsuli aina ya Cloxacillin ambazo zote kwa pamoja Bw. Sillo alizitaja kwamba zina madhara kwa watumiaji ikiwemo kushindwa kupumua na kupoteza Fahamu.

        Katika Hatua Nyingine TFDA imebadili na kudhibiti zaidi matumizi ya aina nne za dawa nchini. Mojawapo ni Dawa ya kutibu malaria aina ya vidonge yenye mchanganyiko wa Sulphadoxine na Pyrimethamine (SP)ambayo imebadilishwa kutoka kutibu malaria na kuwa kinga ya malaria kwa kina mama wajawazito kwa mujibu wa mwongozo wa kisera wa kupima na kutibu Malaria wa mwaka 2013 wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii.

Dawa nyingine zilizodhibitiwa zaidi ni dawa aina ya Kanamycin Amikacin na Levofloxian kwa kuruhusu dawa hizi kutumika kwa ajili ya ugonjwa wa kifua kikuu katika hospitali, vituo vya afya na zahanati pekee. Bw. Sillo alieleza sababu ya kudhibiti zaidi ni kuzuia usugu wa vimelea vya bacteria vya ugonjwa wa Kifua kikuu.

      Aidha, Bwana Sillo ametoa wito kwa wamiliki wa maduka ya Dawa pamoja wananchi kuzingatia taarifa hizi za kiudhibiti kwa lengo la kuepuka madhara yanayoweza kutokea kutokana na matumizi ya dawa hizo. Sillo alizitaka Hospitali mbalimbali nchini pamoja maduka ya dawa kuaacha kuuza dawa hizo mara moja na kuzirudisha walikozinunua kwa ajili ya kuziteketeza.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...