KATIKA kuhakikisha kuwa 93.7 Efm inaendeleza utamaduni wake wa kushirikiana na wasikilizaji kama familia, inatoa nafasi nyingine tena ya kuwawezesha kiuchumi kupitia shindano lake la sakasaka ambalo limeanza rasmi jana Kigamboni jijini Dar es salaam.
Shindano hili linawawezesha washiriki ambao ni wasikilizaji wote  wa EFM,  kujishindia zawadi ya fedha taslimu kuanzia milioni moja na nusu, laki moja na shilingi elfu hamsini kwa lengo la kusonga mbele na wasikilizaji wake kwa kukuza uchumi wa mtu mmoja mmoja  kama shukrani pia ya kuwa wasikilizaji wetu.
Washindi wa shindano hilo wamegawanyika katika maeneo matatu, ambapo kila wiki mshindi mmoja atajinyakulia kitita cha shilingi milioni moja na nusu, washindi watatu wataondoka na laki moja kila mmoja na wengine wanne watajinyakulia shilingi elfu hamsini kwa kila mmoja.
Hatua hii inakuja baada ya kituo hicho kuhitimisha maadhimisho yake ya mwaka mmoja ambayo yalitoa gari mbili za biashara na kuhitimishwa na Tamasha kubwa la miaka 16 ya msanii wa musiki wa kizazi kipya Juma Nature, lakini pia kuwajazia mafuta wale wote wenye stika za efm katika vyombo vyao vya usafiri ikiwemo boda boda, bajaji na gari.
“Kikubwa zaidi ambacho tunakisisitiza kwa msikilizaji wetu kuwa hili shindano la sakasaka linamlenga kila mtu anayesikiliza matangazo yetu kuanzia asubuhi hadi jioni kila siku na jana tumeanza na wilaya ya Temeke ambayo itafuatiwa na Wilaya za Ilala na Kinondoni”  Amesema Dennis Ssebo, Meneja Mahusiano na Mawasiliano machachari kabisa wa 93.7 wa EFM.
Mfumo mzima wa shindano hilo unamtaka msikilizaji kufuatilia matangazo ya efm ili kujua fedha hizo zimefichwa wapi ili aweze kujinyakulia vitita hivyo.    
 Kijana wa Temeke afurahia baada ya kusaka na kufanikiwa kupata mahela ya 93.7 EFM mwishoni mwa juma katika mambo ya Sakasaka
 Zote hizi zangu kweli???
 Sakasaka ikiendelea Temeke
 Sakasaka hadi juu ya miti na kila kona....

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...