Mwanafunzi wa Chuo kikuu cha Dar es Salaam mwaka wa tatuMwakijangile Frank akipiga shuti kali kuelekea katika goli la wanafunzi wa mwaka wa pili wakati wa Tamasha la”Back to School Bash” lililofanyika kwenye viwanja vya Mabibo Hosteli jana lililoandaliwa na Vodacom Tanzania,Ambapo mwaka wa pili walifungwa 2-1.
Mshambuliaji wa timu ya mwaka wa tatu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam,Charles Mgao(katikati) akijaribu kuwatoka Mabeki wa timu ya mwaka wa pili wakati wa Tamasha la”Back to School Bash” lililofanyika kwenye viwanja vya Mabibo Hosteli jana lililoandaliwa na Vodacom Tanzania,Ambapo mwaka wa pili walifungwa 2-1.
Msanii wa muziki wa Kufokafoka”Hip Hop”Roma Mkatoliki, akikonga nyoyo za mashabiki wake wakati wa Tamasha la”Back to School Bash” lililofanyika hapo jana katika viwanja vya Mabibo Hosteli jijini Dar es Salaam kwa Udhaminiwa wa Vodacom Tanzania.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...