Mkuu wa Wilaya ya Bukombe ambaye pia ni mwenyekiti wa kamati ya Ulinzi na
Usalama ya Wilaya anapenda kuwatangazia Wananchi wa Bukombe na umma wote
kwa ujumla kuwa maandamano yaliyoitishwa na Chama cha Walimu Wilayani hapa
ambayo yanatarajiwa kufanyika tarehe 18/05/2016 ni batili na hayana msingi wowote
kwani hoja zote 17 ambazo waliziorodhesha zilishajibiwa na Mkurugenzi wa
halmashauri ya Wilaya ya Bukombe kupitia barua yenye Kumb. Na. A.30/3/84 ya tarehe
16/05/2016.
Aidha Mkuu wa Wilaya amekitaka chama cha Walimu kama hakikuridhishwa na majibu
ya hoja zao, bado kina nafasi ya kukutana tena na Mkurugenzi wa Halmashauri ya
Wilaya na Kuzungumzia masuala hayo badala ya kufanya maandamano ambayo
yataathiri shughuli za mitihani ya “Mock” kwa kidato cha nne iliyoanza tarehe 10 hadi
20/05/2015 na ile ya “STEP” chini ya BRN kwa shule za sekondari iliyoanza tarehe 16
hadi 20/05/2016.
Kamati kuu ya Ulinzi na usalama ipo imara kudhibiti maandamano hayo na vitendo
vyovyote vinavyoashiria uvunjifu wa Amani katika Wilaya ya Bukombe.
Imetolewa na:
Ofisi ya Mkuu wa Wilaya Bukombe
Geita
17 Mei, 2016
Siwaachiwe tu waandamane tusikie kipi kipya. Waandamane siku ya Jumapili ama Jumamosi, sio siku ya kufundisha. Kuwakatalia kufanya maandamano ya amani si sahihi hata kama shida za 17 zimetekelezwa. Hata hiyo moja inaweza kuwa halali kufanya maandamano.
ReplyDelete