Na  Bashir  Yakub.

1.NINI MAANA  YA  KUUMIA  KAZINI.

Kuumia  kazini  kunajumuisha  kila  jeraha  analolipata  mfanyakazi  wakati  akitekeleza  majukumu  yake  ya  kazi. Jeraha  laweza  kuwa  dogo  au  kubwa   lakini  litaitwa jeraha  tu. Katika maana  hii  yapo  mambo mawili  kwanza  jeraha  na  pili   wakati  ukiwa  kazini.  Ili  mfanyakazi  apate  stahiki  zake  ni  lazima  haya mawili  yatokee.

( a ) JERAHA  HUJUMUISHA  NINI.

Jeraha  ni  pamoja  na  kidonda, kukatika  kiungo iwe  mkono ,  mguu,  kidole  au  vinginevyo, kuathirika  akili, magonjwa yaliyotokana  na  kazi  kwa  mfano  kansa  inayotokana  na  kemikali  za  viwanda, magonjwa  ya  ngozi, na athari  nyingine  za  kimwili  au  kiakili  zilizotokea   wakati  mfanyakazi  akiwa  kazini au  zilizosababishwa na  kazi   ya  mfanyakazi. 

( b ) NI  WAKATI  UPI  NI  WA  KAZI.

Wakati  wa  kazi  ni  wakati  wote  ambao  mfanyakazi  atakuwa  akitekeleza  majukumu  yake  ya  kazi kwa  mujibu  wa  ratiba  ya  ofisi. Kuumia  ukitekeleza  kazi  za  kiofisi  nyumbani  kwako  hakuwezi  kuhesabika   kama  kuumia  kazini /wakati  wa  kazi. 

Lakini  kuumia  ukiwa  safarini  kuelekea  mkoa  au  nchi  fulani  kutekeleza  majukumu  ya  kazi  ni  kuumia  wakati  wa  kazi.  Hii  ndiyo  tafsiri  yake.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 18, 2016

    Hongeara sana kwa kazi nzuri ya kuelimisha jamii yetu.
    Ila pia tunaomba utupe darasa la wanaoumia wakiwa kwenye magari ya binafsi au ya abiria.

    Maana nchi za wenzetu ukiumia ndani ya magari ya abiria bima zao zinatoa malipo ya pesa za hospital(matibabu ) na pesa za kujikimu kimaisha wakati unajiuguza kabla ya kurudi kazini. Lakini sijawahi ona Watanzania wanalipwa malipo kama haya kwenye ajali nyingi zinazotokea.

    Hii itasababisha wananchi kudai haki zao kupitia bima ya gari pindi ajali zinapotokea.Pia itafanya madereva kuwa makini wakiwa na abiria.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...