MAHAKAMA kuu ya Tanzania kanda ya Iringa imemhukumu kwenda jela miaka 15 askari Polisi Kikosi cha Kutuliza Ghasia ( FFU ) Iringa namba G 58 Pacificius Cleophace Simon (27) kwa kosa la kumuua bila kukusudia mwanahabari Daudi Mwangosi mwaka 2012 katika kijiji cha Nyololo wilaya ya Mufindi, wakati akiwa katika majukumu yake ya kikazi. 



Akisoma hukumu hiyo, Jaji Dkt. Paul Kihwelo, alisema kuwa mshitakiwa amekutwa na hatia hiyo ya kuua bila kukusudia katika shitaka la pili lililosomwa Mahakamani hapo hii leo, baada ya shitaka la kwanza kusomwa na kukutwa hana hatia.


Kesi hiyo ilianza kusikilizwa mwezi Februari 12, 2015, na kufikia hukumu hiyo ya kumtia hatiani hii leo. Tukio hilo lilitokea 2/9/2012 katika kijiji cha Nyololo wilaya ya Mufindi, Mkoa wa Iringa.
Mjane wa marehemu Daudi Mwangosi Itika Mwangosi (wa tatu kulia) akiwa na baadhi ya wanandugu katika foleni ya ukaguzi wa polisi kuingia Mahakamani husikiliza Hukumu ya Askari Polisi.
Mjane wa marehemu Daudi Mwangosi Itika Mwangosi (kulia) akifurahia jambo na ndugu yake mzee Marko Mfugale mahakamani hapo leo.
Rais wa umoja wa klabu za waandishi wa habari Tanzania Bw Deo Nsokolo akizungumza na wanahabari baada ya hukumu ya kesi hiyo.
Picha na Francis Godwin, Iringa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...