Na. Immaculate Makilika Dodoma
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mheshimiwa Jenista Mhagama amesema kuwa kufanyika kwa maombolezo ya kumbukumbu za Mashujaa inawakumbusha watanzania kuwa wazalendo.
Akizungumza wakati wa maombolezo ya kumbukumbu za Mashujaa sambamba na kuwashwa kwa Mwenge wa Uhuru katika mnara wa kumbukumbu za Mashujaa, leo usiku katika viwanja wa Mashujaa vilivyopo mjini Dodoma, Waziri Mhagama alisema kuwa kufanyika kwa maombolezo ya Mashujaa mkoani Dodoma ni heshima kwa wananchi wa Dodoma na watanzania wote kwa ujumla.
“Kufanyika kwa maombolezo haya inatukumbusha watanzania kuwa wazalendo na kupigania bila kuchoka, bila kujali makabila yetu na tujifunze kwa Mashujaa hawa waliopigania uhuru wetu” alisema Waziri Mhagama.Waziri Mhagama aliwaomba watanzania kutumia siku ya kumbukumbu ya Mashujaa ambayo ni Julai 25, kwa namna mbalimbali ikiwemo kufanya maombi ya sala kwa Mashujaa wote walifariki katika harakati mbalimbali za kupigania uhuru wa Taifa la Tanzania.
Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mheshimwa Jordan Rugimbana aliishukuru Serikali kwa uwamuzi wa kuadhimisha kumbukumbu za mwaka huu za Mashujaa mkoani Dodoma, na kusema kuwa kufanyika kwa tukio hilo la kihistoria linakumbusha uwajibu wa watanzania na Mkoa wa Dodoma utaienzi heshima hiyo.
Aidha, Mkuu wa Wilaya ya Dodoma mjini Mheshimiwa Christina Mndeme aliwasha Mwenge wa Uhuru katika kilele cha mnara wa mashujaa mnano saa 6 kamili usiku ikiwa ni sehemu ya maombolezo ya kumbukumbu ya Mashujaa.Mnara wa Mashujaa uliopo mkoani Dodoma ni kati ya vituo 4 vilivyopo nchi nzima ambavyo vimekuwa na makaburi ya Mashujaa mbalimbali waliopigania uhuru wa nchi ya Tanzania. Vituo vingine vipo meneo ya Mtwara, Dar es Salaam na Kagera.
Maadhimisho ya kumbukumbu za Mashujaa kwa mwaka huu yanatarajiwa kufanyika kesho julai 25, mkoni Dodoma ambapo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli atakuwa mgeni rasmi.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mheshimiwa Jenista Mhagama amesema kuwa kufanyika kwa maombolezo ya kumbukumbu za Mashujaa inawakumbusha watanzania kuwa wazalendo.
Akizungumza wakati wa maombolezo ya kumbukumbu za Mashujaa sambamba na kuwashwa kwa Mwenge wa Uhuru katika mnara wa kumbukumbu za Mashujaa, leo usiku katika viwanja wa Mashujaa vilivyopo mjini Dodoma, Waziri Mhagama alisema kuwa kufanyika kwa maombolezo ya Mashujaa mkoani Dodoma ni heshima kwa wananchi wa Dodoma na watanzania wote kwa ujumla.
“Kufanyika kwa maombolezo haya inatukumbusha watanzania kuwa wazalendo na kupigania bila kuchoka, bila kujali makabila yetu na tujifunze kwa Mashujaa hawa waliopigania uhuru wetu” alisema Waziri Mhagama.Waziri Mhagama aliwaomba watanzania kutumia siku ya kumbukumbu ya Mashujaa ambayo ni Julai 25, kwa namna mbalimbali ikiwemo kufanya maombi ya sala kwa Mashujaa wote walifariki katika harakati mbalimbali za kupigania uhuru wa Taifa la Tanzania.
Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mheshimwa Jordan Rugimbana aliishukuru Serikali kwa uwamuzi wa kuadhimisha kumbukumbu za mwaka huu za Mashujaa mkoani Dodoma, na kusema kuwa kufanyika kwa tukio hilo la kihistoria linakumbusha uwajibu wa watanzania na Mkoa wa Dodoma utaienzi heshima hiyo.
Aidha, Mkuu wa Wilaya ya Dodoma mjini Mheshimiwa Christina Mndeme aliwasha Mwenge wa Uhuru katika kilele cha mnara wa mashujaa mnano saa 6 kamili usiku ikiwa ni sehemu ya maombolezo ya kumbukumbu ya Mashujaa.Mnara wa Mashujaa uliopo mkoani Dodoma ni kati ya vituo 4 vilivyopo nchi nzima ambavyo vimekuwa na makaburi ya Mashujaa mbalimbali waliopigania uhuru wa nchi ya Tanzania. Vituo vingine vipo meneo ya Mtwara, Dar es Salaam na Kagera.
Maadhimisho ya kumbukumbu za Mashujaa kwa mwaka huu yanatarajiwa kufanyika kesho julai 25, mkoni Dodoma ambapo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli atakuwa mgeni rasmi.
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mh. Jordan Rugimbana akiongea na baadhi wa viongozi wa serikali waliohudhuria tukio hilo la uwashwaji wa Mwenge na kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuupa heshima Mkoa wa Dodoma wa kuadhimisha siku ya mashujaa.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama akiongea na baadhi wa viongozi wa serikali waliohudhuria tukio hilo la uwashwaji wa Mwenge na kutoa rai kwa watanzania kuwa wazalendo na nchi yao bila kujali itikadi ya mtu kama walivyofanya wazee wetu waliopigania uhuru wa nchi.
Baadhi ya Viongozi mbalimbali wa Serikali wakishuhudia uwashwaji wa Mwenge. PICHA NA HASSAN SILAYO ,
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...