Watanzania wawachangia wahanga wa tetemeko Kagera,zaidi ya laki 4 kupitia huduma ya M-Pesa mara baada ya kuzinduliwa kwa kampeni ya uchangiaji ya”Red Alert”inayoendeshwa na Vodacom Tanzania,Kampuni hiyo ilikabidhi jumla ya sh.milioni 100/- kwa Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kwa ajili ya waathirika wa tetemeko la ardhi lilitokea kanda ya ziwa septemba 10 mwaka huu.
Akizungumza jijini Dar es salaam jana Mkuu wa kitengo cha Vodacom Tanzania Foundation, Renatus Rwehikiza alisema kati ya fedha hizo zilizochangwa mara baada ya kuzinduliwa kwa kampeni ya uchangiaji wa waathirika wa tetemeko hilo sh. Mil 99.51 zilitolewa na kampuni yake na sh. 490,000 zilichangwa na watanzania kupitia M-Pesa.
“Kiasi kilichochangwa na wasamaria wema ni sh 490,000 na sisi Vodacom tukatoa sh,mil 99.51 ambazo zilijumlimshwa na kupatikana sh mil 100/-ambazo hundi yake ilikabidhiwa kwa Waziri Mkuu Septemba 24 mwaka huu na Mkurugenzi mtendaji wa Vodacom Tanzania,Ian Ferrao mara baada ya kampeni ya uchangiaji kuhitimishwa”alifafanua Rwehikiza.
Aidha Rwehikiza alibainisha kuwa awali Taasisi yake ilipanga kununua vifaa mbalimbali kwaajili ya kuwasaidia waathirika hao lakini kwa kuwa Kamati ya Maafa Bukoba ambayo ipo chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu Kitengo cha Maafa ilikuwa na uhitaji wa fedha zaidi tuliona ni bora tukabidhi fedha.
Katika hatua nyingine Rwehikiza alitoa wito kwa watanzania ,mashirika na Taasisi mbalimbali nchini kuendelea kujitoa katika kuchangia waathirika wa tukio hilo badala ya kuiachia serikali pekee kwani bado uhitaji ni mkubwa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...