Na Mwandishi wetu.
BODI ya Filamu Tanzania leo imemkabidhi cheti na hundi yenye thamani ya shilingi Laki Mbili mwanafunzi Omary Maganga aliyefanya vizuri kwenye masomo ya filamu na runinga kutoka Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TASUBA).
Makabidhiano hayo yamefanyika kwenye ofisi za bodi hiyo ambapo Afisa Uhusiano na Mawasiliano Abuu Kimario alimkabidhi cheti hicho na hundi kwa niaba ya Katibu Mtendaji Joyce fisoo.
Baada ya kukabidhiwa zawadi zake bwana Maganga aliishukuru Bodi hiyo ya filamu kwa kutambua juhudi za wanafunzi wanaofanya vizuri kwenye masomo yao. Pia ameziasa taasisi zingine za Serikali na zisizo za kiserikali kuwatambua wanafunzi wanaofanya vizuri kwani kwa kufanya hivyo kunaongeza morali na ushindani.
Wakati huo Afisa Uhusiano na Mawasiliano Abuu Kimario kwa niaba ya Katibu Mtendaji wa bodi hiyo ametoa ahadi ya kuendelea kutoa zawadi kwa wanafunzi wanaofanya vizuri kwenye masomo yenye uhusiano na tasnia ya filamu.
Kwa sasa Bodi ya Filamu Tanzania iko kwenye utekelezaji wa programu ya kutambua na kukuza vipaji vya wanafunzi wanaofanya vizuri kwenye masomo ya tasnia ya filamu nchini. Program hii ilianzishwa ikiwa na lengo la kukuza ubora wa filamu za Kitanzania.
Hongera kijana... Tunahitaji mabadiliko katika filamu zetu, tunawaamini kwa pamoja mtaweza.
ReplyDeleteHongera sana kaka Maganga, dah safi aisee nakumbuka jitihada zako wakt tupo sote Hostel,keep moving nakumbuka dream yako ya kutaka kuwa James Cameron Director mkubwa Duniani kila kitu kinawezekana jitihada tuu kaka
ReplyDeleteHongera sana tupo pamoja