Habari picha na Woinde Shizza,Arusha 
Bendi mpya ya mziki wa dance ijulikanayo kwa jina la Mount Meru Ricknest music bandi imezinduliwa rasmi mkoani Arusha ikiwaahidi wapenda mziki wa dance burudani isiokuwa na mpinzani. 
Akiongea na waandishi wa habari jana mmoja wa wakurugenzi wa bendi hiyo Ernest mlolere alisema kuwa kwa sasa wameitambulisha bendi hiyo kwa wakazi wa mkoa wa Arusha tu na wanatarajia kuzindua bendi hiyo rasmi katika siku ya wapendanao (valentine day ) hapa hapa jijini Arusha. 
Alibainisha kuwa bendi hiyo ipo chini ya wakurugenzi watatu akiwemo yeye mwenyewe Ernest Mlolere, Denis Kaiza pamoja na Prisca Aloyce ambapo wamekaa chini na wakaamua kuanzisha bendi hiyo ili kuweza kuwapa burudani wakazi wa mkoa wa Arusha ambao wamekuwa wakikosa burudani ya bendi ya uhakika kwa muda mrefu. 
Alisema kuwa kumekuwa na bendi jijini hapa lakini zimekuwa hazikoshi nyoyo za wapenzi wao wa musiki wa dance hivyo wameona wawaletee wanamusiki wenye uzoefu, wenye vipaji vya kutosha ili wananchi wa mkoa wa Arusha pamoja na jirani kuweza kupata burudani. 
 Rais wa bendi ya  Mounti Meru Rickernest Music Band Fabrice Kinyenya (kulialia) Akiwa anaimba katika usiku wa kuwatambulisha bendi hiyo wakazi wa jiji la Arusha
 wanamusiki wa bendi ya Mounti Meru Rickernest Music Band wakiwa wanaonyesha kiwango chao ndani ya ukumbi wa Triple A jijini Arusha
 Wanenguaji wa bendi ya Mount meru Rickernest Music Band wakifanya yao. Kwa habari kamili BOFYA HAPA



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...