Mwalimu wa shule ya sekondari Ndugu,Wilaya ya Mbozi mkoa wa
Songwe,Christian Kiyeyeu mwenye umri wa miaka 31 ameibuka mshindi baada
ya kubashiri vyema matokeo ya mechi kupitia Kampuni ya M-Bet na
kujishindia kitita cha Shilingi Milioni 30/-.
Kiyeyeu amekabidhiwa fedha zake leo katika hafla fupi iliyofanyika jijini Dar es Salaam kwenye ofisi za M-Bet
Kwa upande wake, Msemaji wa M-Bet, Godluck Wambura
alisema kuwa Kiyeyeu alifanikiwa kuzoa kitita hicho baada ya kufanikiwa
kutabiri matokeo ya mechi…. za ligi ya Ulaya kwa mtindo wa kucheza
kawaida.
“Tumefurahi kumkabidhi mshindi wetu kitita hichi cha
Sh milioni 30/- akiwa ndiye mshindi wa M-Bet ambapo amesema ataiwekeza
katika biashara zake na kuweza kumalizia nyumba yake ambayo tayari
alikwishaanza kuijenga,” alisema Wambura.
Aliwataka watanzania kuchangamkia kutumia mtandao wa
intaneti kuonyesha ushabiki halisi wa soka akisema kuwa Perfect 12 na
michezo mingine ni michezo mizuri inayoweza kubadilisha maisha yako mara
moja ukiwa umelala masikini na kuamka tajiri kwa kutabiri kwa kiasi cha
Tsh 1,000 tu unaoruhusu kutabiri mechi 12 kwa mchezo wa perfect 12
ambapo ukipatia zote unaondoka na kitita chako mchana kweupe.
Naye Mshindi huyo, Christian Kiyeyeu amewashauri
watanzania wote hususani walimu wenzake wenye umri unaoruhusiwa kisheria
kujitokeza kubashiri matokeo ya mechi mbalimbali kupitia Kampuni ya
M-Bet .
"Nashukuru sana M-Bet kwa kuniwezesha kujikwamua
kimaisha, nitatumia fedha hizi kutimiza ndoto yangu ya kumalizia nyumba
yangu kwa ujenzi", alisema Kiyeyeu.
Kuhusu m-Bet, ni Kampuni iliyosajiliwa chini ya
Sheria za Tanzania na kupewa leseni na Bodi ya Michezo ya kubahatisha
tanzania kwa lengo la kufanya upatikanaji rahisi na mwingiliano wa
huduma ya mchezo wa kubahatisha (Sim Betting) nchi nzima.
Meneja wa huduma kwa wateja wa M-bet, Jaykishan
Kaba (kushoto)akimkabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi
Milioni 30/- mshindi wa M-bet, Mkazi wa mkoa wa Songwe,Christian
Kiyeyeu(kulia)katika hafla fupi ya makabidhiano hayo yaliyofanyika jijini
Dar es Salaam mwishoni mwa wiki,Katikati ni Msemaji wa M-bet
Gudluck Wambura.
Meneja wa huduma kwa wateja wa M-bet,Jaykishan
Kaba(kushoto) na mshindi wa M-bet, Mkazi wa mkoa wa
Songwe,Christian Kiyeyeu(kulia)wakimsikiliza Msemaji wa M-bet
Gudluck Wambura,akifafanua jambo kwa waandishi wa habari(hawapo
pichani) wakati wa hafla fupi ya kumkabidhi hundi yenye thamani ya
shilingi Milioni 30/- mshindi huyo jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...