Rais wa Marekani Donald Trump amewafuta kazi mabalozi wote wa nchi hiyo kote duniani na wanaohudumu katika mashirika ya kimataifa.
Kwa mujibu wa taarifa ya mtandao wa Independent, mabalozi hao wametakiwa kuachia nafasi zao mara moja na kurudi nyumbani.

Kiongozi huyo juzi alifanya ziara yake ya kwanza katika ofisi za makao makuu ya shirika la Ujasusi la Marekani CIA, na kuvituhumu baadhi ya vyombo vya habari nchini humo wakati akitoa hotuba yake, kwamba vinawagawa wananchi.

Zaidi ya mabalozi 80 wa Marekani katika nchi mbali mbali duniani walifutwa kazi Ijumaa tarehe 20 Disemba saa sita mchana punde baada ya Trump kuapishwa.

Hatua hiyo ya Trump inatazamiwa kuvuruga uhusiano na wa itifaki muhimu kama vile Ujerumani, Uingereza, Canada. Inatabiriwa kuwa nchi hizo zinaweza kukaa bila mabalozi kwa miezi kadhaa kwani baada ya Trump kuteua mabalozi wapya watalazimika kuidhinishwa na Bunge la Kongresi kabla ya kuanza kazi zao.

Source: Independent

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...