KAMPUNI za ujenzi nchini zimeshauriwa kuungana na kushirikiana na kampuni za ujenzi kutoka China ili kujifunza namna wanavyofanya kazi kwa ufanisi.

Akizungumza ofisini kwake jijini Dar es Salaam jana, Katibu Mkuu wa Asasi ya Ushirikiano kati ya Tanzania na China, Bwana Joseph Kahama alibainisha kuwa kampuni za ujenzi nchini bado zina safari ndefu ya kuongeza ujuzi na mbinu za kibiashara.

“Wachina ndio wanaoongoza katika ujenzi duniani, mataifa mengi yaliyoendelea majengo yao yanasimamiwa na kampuni za kichina, hivyo hakuna namna kwa kampuni za Kitanzania kushindana nazo wakitaka kufanikiwa wajipenyeze na kuomba ushirikiano hapo watajifunza mengi.

“Kujifunza kuna njia nyingi, ni utaratibu mzuri katika biashara kujipanga,” alisisitiza Bw. Kahama na kuongeza: “zaidi ya asilimia 80 ya kampuni kubwa za ujenzi duniani zinatoka China, na hapa nchini zipo nyingi kwa sasa huu ndio wakati wetu wa kuchota ujuzi.”

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya China Civil Engineering Construction Corporation (CCECC East Africa Limited), Bwana Yigao Jiang alisema kampuni yake imekuwepo nchini tangu miaka ya 1960 na wapo tayari kuwasaidia Watanzania katika nyanja zote ikiwemo masuala ya kijamii.
Mkuu wa wilaya ya Chato, Bw Elias Makory akimkabidhi cheti Mkurugenzi wa Operesheni wa kampuni ya China Civil Engineering Construction Corporation (CCECC) Bw.An Yi kwa kutambua mchango wa kampuni hiyo kwa jamii mara baada ya kupokea madawati 50 kwa matumizi ya wanafunzi 150. Kampuni hiyo imeshatoa jumla ya madawati 150 yenye thamani ya milioni 30 na itaendelea kuchangia huduma mbalimbali za kijamiii.
Mkuu wa wilaya ya Chato, Bw Elias Makory (wapili kushoto) akipokea rasmi madawati 50 toka kwa Mkurugenzi wa Operesheni wa kampuni ya China Civil Engineering Construction Corporation (CCECC) Bw.An Yi (watatu kushoto). Kampuni hiyo imeshatoa jumla ya madawati 150 yenye thamani ya milioni 30 na itaendelea kuchangia huduma mbalimbali za kijamiii.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...