Na Jacquiline Mrisho – MAELEZO.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Kebwe S. Kebwe ametoa rai kwa vijana kujiweka katika vikundi ili wapate fursa za kupata mikopo kutoka Serikalini na kwa wadau mbalimbali. 

Mkuu wa Mkoa ametoa rai hiyo leo mkoani Morogoro alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hii juu ya maendeleo ya vijana wenye ulemavu waliopo chini ya Mradi wa Uwezeshaji Vijana Kiuchumi (YEE) unaoratibiwa na shirika la Plan International.

Mhe. Kebwe amesema suala la vijana na wanawake kuunda vikundi ni la muhimu kwani Serikali kupitia Halmashauri zote nchini ina utaratibu wa kutenga asilimia kumi kutoka katika mapato ya ndani ya Halmashauri husika kwa ajili ya kuwasaidia wanawake na vijana ili waweze kujikwamua hasa katika nyanja ya kiuchumi.

“Serikali pekee haiwezi kufanya kila kitu hivyo kupata mradi kama huu wa kuwasaidia vijana kiuchumi kutoka Umoja wa Ulaya ni fursa nzuri kwa vijana kujikomboa na njia rahisi ya kuoneka mna uhitaji ni dhahiri kuwa mnatakiwa muwe katika vikundi,”alisema Mhe. Kebwe.

Mhe. Kebwe ameongeza, uundwaji wa vikundi unasaidia kufahamu ukubwa wa kikundi, kiasi cha msaada, eneo kikundi kilipo na aina ya shughuli inayofanywa na kikundi husika.

Amefafanua kuwa kwa hali halisi fedha za mradi haziwezi kutolewa kwa mtu mmoja mmoja bali ni kwa njia ya vikundi ili kurahisisha ufatiliaji na kupunguza gharama za uendeshaji hivyo vijana wasitarajie kupata mkopo au kusaidiwa na shirika wakiwa wamekaa vijiweni.

Aidha,amewasisitiza vijana hasa walemavu kujitokeza kwa wingi katika awamu ya mwisho ya mradi huo kwani mradi huo upo kwa ajili ya vijana wote.

Mradi huo wa miaka mitatu (2015/2018) unatekelezwa kwa ushirikiano wa mashirika ya VSO, CCBRT, VETA, UHIKI, CODERT pamoja na Serikali ya Tanzania huku ukiratibiwa na Shirika la Plan International chini ya ufadhili wa Umoja wa Nchi za Ulaya (EU).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...