Ubalozi wa Kuwait unaendelea kuiunga mkono Shule ya Sekondari ya Tolido iliyopo Tanga kwa kuipatia idara ya shule hiyo mashine ya kutoa kopi(photocopy machine) iliyopokelewa na msimamizi wa Shule Bi, Basilisa Soka.

Mashine hiyo inatarajiwa kuisaidia Shule na kurahisisha kazi za idara kwa ajili ya kuinua kiwango cha elimu.

Itakumbukwa kuwa Balozi wa Kuwait nchini Mhe.Jasem Al-Najem alizindua kisima cha maji katika shule hiyo mwishoni mwa mwaka jana 2016 ambapo mradi wa ujenzi wake ulifadhiliwa na Msamaria mwema raia wa Kuwait na kutekelezwa na Asasi ya Direct Aid-ofisi ya Tanga, kisima hicho ndio cha kwanza kuzinduliwa tangu ubalozi wa Kuwait kuzindua mpango wake wa 'Kisima cha maji kwa kila Shule'.

Idadi ya visima ambavyo tayari vimezinduliwa ndani ya mpango huo vimefikia visima 27 katika shule mbalimbali katika kipindi cha miezi minne tu.

Ubalozi wa Kuwait utaendela kuisaidia Shule ya Tolido ya Sekondari mjini Tanga na shule nyingine Tanzania ili kuunga mkono mchakato wa elimu nchini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...