Na Karama Kenyunko blogu ya jamii


Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia , Wazee na Watoto, Dk. Hamis Kigwangalla, amewatunuku vyeti wanafunzi wa kike 25 wa shule mbalimbali za sekondari waliofanya vizuri katika mafunzo ya uchambuzi wa takwimu.

Dk. Kigwangallah ametoa vyeti hivyo leo kwa wanafunzi hao baada ya mafunzo ya siku tatu ya namna ya kutumia takwimu.

Mafunzo hayo yameandaliwa na kufadhiliwa na DataLab-dlab kwa kushirikiana na UDICTII, Apps Girls and She Code for change na yamelenga kuwajengea uwezo kwenye eneo la kutumia takwimu, kuzitafsiri na kuziweka kwenye taarifa ambazo zinaweza kutumika na walaji kama vile wanahabari, wabunge, watunga sera na wengine wenye uhitaji.

Dk. Kigwangallah amewapongeza waandaji na kueleza kuwa yatawajenga watoto kwenye utamaduni wa kutumia takwimu.

Mkuu wa Mafunzo wa Mradi wa Takwimu, Tanzania, Mahadia Tunga, ambaye ni Mhadhiri Msaidizi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam, amesema wameamua kutoa mafunzo hayo ya uchambuzi wa takwimu kwa watoto wa kike sababu mara nyingi mwamko wao huwa ni mdogo tofauti na wanaume.

Amesema kuwa mafunzo hayo wanayatoa kwa watoto kuanzia umri wa miaka 15 hadi 20 ili kuwajengea uwezo wa kukabiliana na changamoto na kuzipatia ufumbuzi.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kigwangalla akikabidhi Zawadi kwa Mwanafunzi wa kidato cha tano shule ya Sekondari ya Benjamini Mkapa ambaye ni mshindi wa kwanza wa Data Innovation, Asha Abbas.
Wasichana Walioshiriki katika Mafunzo wakifatilia hotuba ya Naibu waziri.

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...