Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Mashaka Gambo ametaka kurejeshwa kwa aliyekuwa Mkurugenzi wa Jiji Ndg. Juma Iddi, Mwekahazina Kessy Mpakata pamoja na Dr. Bakari Salum ambao wataungana na Katibu wa Afya Optat Ismail ili kujibu tuhuma zinazowakabili za ubadhirifu wa Fedha za mfuko wa pamoja wa kapu la Afya (Busket Fund). 

Gambo ameyasema hayo katika siku ya kwanza ya ziara yake Jijini hapa ambapo alikuatana na wafanyakzi wa Jiji, Taasisis za Serikali, Bodi na Kamati za Shule, Viongozi wa Dini, Wazee wa Mji pamoja na Makundi Maalum. 

Alisema kuwa amefikia uamuzi huo baada ya kupokea Taarifa ya Tume aliyoiunda kukagua matumizi ya mfuko huo wa Afya endapo taratibu zilizingatiwa katika mapato na matumizi na kama Fedha hizo ziliwafikia wananchi kupitia huduma bora za Afya. 

Aliongeza kusema kuwa kupitia Taarifa ya Tume hiyo alibaini ubadhirifu wa Fedha hizo kwani zilipelekwa kwenye Hospital ya St. Elizabert pamoja na Isnasheer pasipo kuwa na Mikataba inayoeleweka na mikataba mingine kutokuonekana kabisa hivyo kuwa na mashaka na matumzi ya Fedha hizo na manunuzi ya madawa kufanyika pasipo kuwa na risit za kielektroniki. 

“Alisema kuwa haiwezekana Fedha zitumiwe kana kwamba hakuna miongozo wala maelekezo ya Serikali kwa sababu Hospital zingine zimekwisha fungwa lakini bado inaonekana Fedha zilipelekwa sasa sijui zilikuwa zinatumiwa kwenye eneo gani wakati Hospital Haifanyi Kazi” 

Rc Gambo pia alimuagiza Mkurugenzi wa Jiji Ndg. Athumani Kihamia kuwasimamisha Kazi watumishi 23 wa Timu ya Menegimet ya Afya(CHMT) kupisha uchunguzi wa matumizi ya Tsh Mil 63 walizojilipa posho pasipo kuwa na Taarifa ya kazi(Activity report). 

Ziara hii za siku tabo itahusisha uzinduzi na uwekaji na ufunguaji wa miradi ya maendeleo, mikutano ya hadahara pamoja na kutatua kero za wananchi wa Jiji hili. 

Nteghenjwa Hosseah 

Afisa Habari, Halmashauri ya Jiji 

Arusha. 

26 April 2017
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Mashaka Gambo akiongea kwenye kikao wakati wa siku ya kwanza ya ziara yake Jijini hapa. 
Watumishi wa Jiji, Taasisi za Serikali, Viongozi wa Dini pamoja na wazee wakimskiliza Mkuu wa Mkoa (hayupo pichani) wakati wa ziara yake Jijini hapa. 
Mkuu wa Wilaya ya Arusha Gabriel Daqarro akiwasilisha Taarifa ya Wilaya wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa Jijini Arusha 
Baadhi ya Viongozi wa Dini waliohudhuria Kikao cha Mkuu wa Mkoa wa Arusha 
Watumishi wa Jiji la Arusha wakifuatilia Kikao cha Mkuu wa Mkoa. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...