Nenda Yusuf,Imetosha na ahsante sana,najua ni maamuzi magumu lakini naamini sasa ni wakati wa akili kubwa kufanya kazi kwa bidii na nina wakati wa kumrudisha kundini Dr Jonas Tiboroha na kuja kuongeza nguvu na Katibu mKuu Mkwassa na hakika tutasogea mbele zaidi
Mengi yemeongewa na kusemwa na naamimi mengine ni ukweli mtupu na mengine ni porojo ila naamini kuna mapungufu makubwa katika uongozi wako uliopita na kubwa zaidi ya yote ni kamati ya utendaji kukosa meno ya nguvu ya kuhoji mambo kadha wa kadha juu ya matumizi na udhamini,mara kadhaa wale waliokuwa wanahoji tumeona wakifanyiwa fitina na kutolewa nje,wapo wakina Aaron Nyanda,Bin Kleb,Seif Magari,Salum Mkemi nk hapo haikuwa sawa,lazima ifike pahali tukubali kutofautiana mawazo ili tuweze kupiga hatua.
Kamati ya utendaji isiyoweza kumuhoji Mwenyekiti na maamuzi binafsi ya kukataa wadhamini na kujipa udhamini mkuu kwa bei aliyopanga yeye haikuwa sahihi.

Yanga Sc hii ya Sportpesa inamuhitaji @drjonastiboroha na kamati ya utendaji makini ipige hatua na kuachana na kuomba omba as a super brand it will attracts sponsors all over the places,its all about having the right people.

Yanga needs to be restructured ili kuweza kwenda sawa na speed ya masoko,inahitaji the right person kwa nafasi ya Mkuu wa masoko anayeweza kuja na challenges na kuleta mawazo mapya na ku adopt marketing skills ambazo wenzetu majirani wanafanya mfano Zesco au Sofapaka.
Yanga ina watu wanaoitwa wakuu wa idara za magazetini ambazo hazina tija katika day to day operations na hawa add value kwenye maendeleo ya Yanga.Hii ni timu kubwa sio ya kuomba udhamini,hii ni klabu yenye miaka 82 lets have new ways na kutumia weledi katika uendeshaji.

Yanga inahitaji msemaji na kurugenzi ya mawasiliano makini inayoweza kusimamia social media links na kuweza kufanya kazi bega kwa bega na kurugenzi ya masoko kuuza bidhaa za yanga online pia.

Its time tuwape proffessionals wafanye kazi na kuleta ufanisi...tuache blah blah bana Manji kapita kama walivyopita wakina Gulamali,Verani.

By Mac Temba - Fan wa Yanga Sc

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...