WAZIRI
MKUU Kassim Majaliwa amezitaka benki mbalimbali nchini ikiwemo Benki ya
Maendeleo ya Kilimo kutoa mikopo kwa vikundi vya kilimo ili viweze kupata fedha
za kununulia matrekta.
Amesema
Serikali imedhamiria kuimarisha Sekta ya kilimo ili kwenda sambamba na adhma
yake ya kuwa nchi ya uchumi wa viwanda.
Waziri
Mkuu ameyasema hayo leo (Jumanne, Mei 23, 2017) wakati alipotembelea kiwanda
cha kuunganisha Matrekta URSUS-TAMCO, Kibaha mkoani Pwani.
Amesema
kiwanda hicho kinalenga kuboresha sekta ya kilimo nchini na kuongeza uzalishaji
wa malighafi za viwandani kwa kuwa wakulima watakuwa na zana za kisasa.
Aidha,
amevitaka vyuo vya kilimo nchini kununua matrekta hayo kwa lengo la kufundishia
wanafunzi wake ili wanapohotimu wawe na uwezo wa kutumia zana hizo vizuri na kwenda
kuwasaidia wakulima katika maeneo yao.
Pia
Waziri Mkuu ametoa wito kwa Halmashauri nchini kuendelea kupanga matumizi bora
ya ardhi kwa kutenga maeneo ya kilimo, uwekezaji, makazi, biashara na huduma za
jamii, hivyo kuepuka migogoro ya ardhi kwa siku zijazo.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitazama moja kati ya mtrekta aina URSUS yanayounganishwa kwenye karakana ya TAMCO mjini Kibaha Mei 23, 2017.Kulia kwake ni Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu,Kassim Majaliwa akikagua matrekta aina ya URSUS yanayounganishwa katika karakana ya TAMCO mjini Kibaha Mei 23, 2017. Wengine pichani kutoka kulia kutoka kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa NDC Mlingi Elisha Mkucha, Waziri wa Viwanda, Biahara na Uwekezaji, Charles Mwijage, Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evaresti, Ndikilo na kulia kwake ni Mbunge wa Kibaha mjini Silvestry Koka.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitazama moja kati ya mtrekta aina URSUS yanayounganishwa kwenye karakana ya TAMCO mjini Kibaha Mei 23, 2017. Kulia kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhandisi Evarest Ndikilo. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhandisi Evarest Ndikilo akizungumza wakati Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alipotembelea eneo la uwekezaji la Kamal Industrial Estate lililopo Kerege Bagamoyo Mei 23, 2017.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Dkt. Tito Mwinuka baada ya kutembelea eneo la uwekezaji la Kamal Industrual Estate lililopo Kerege, Bagamoyo Mei 23, 2017
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na baadhi ya viongozi, wabunge na wananchi waliohudhuria wakati alipotembelea eneo la uwekezaji la Kamal Industrial Estate lililopo Kerenge, Bagamoyo Mei 23, 2017.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na baadhi ya viongozi, wabunge na wananchi waliohudhuria wakati alipotembelea eneo la uwekezaji la Kamal Industrial Estate lililopo Kerenge, Bagamoyo Mei 23, 2017. (Picha na ofisi ya Waziri Mkuu).
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...