Mstahiki meya wa Jiji la Dar es salaam Mheshimiwa Isaya Mwita Charles leo amekabidhi rasmi magari mawili aina ya Suzuki Carry maarufu kama (Kirikuu) kwa washindi wa shindano la shika ndinga linaloandaliwa na kuendeshwa na kituo cha utangazaji cha EFM redio, washindi waliopatikana katika fainali iliyofanyika tarehe sita mwezi wa tano mwaka huu katika viwanja vya Tanganyika Packers Kawe Jijini Dar es Salaam.

Mstahiki Meya Mheshimiwa. Isaya Mwita akijiandaa kukabidhi magari hayo.

Mstahiki Meya akitoa pongezi zake kwa washindi Kutoka Kulia ni Meneja mkuu Dennis Busulwa, Mshindi (Michael Peter), akifuatiwa na Mshindi Joyce Daniel pamoja na Rukia Mtingwa Meneja masoko Zantel
Washindi wa shindano hilo wakiwa wameshikilia kadi za gari Kutoka kulia ni Michael Peter na Joyce Daniel
Shamla Shamla zikiendelea
Wasindikizaji wa mshindi Michael Peter kutoka Salasala

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...