Na Shamimu Nyaki - WHUSM

Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe ameipongeza timu ya vijana chini ya miaka 17 “Serengeti Boys” kwa hatua nzuri waliyofikia katika kiwango cha Soka la Afrika kwa kushika nafasi ya pili katika kundi B walilokuwa wanacheza wakati wa michuano ya AFCON iliyomaliziki hivi karibuni Mjini Gabon.

Pongezi hizo zimetolewa jana Jijini Dar es Salaam wakati wa hafla ya kuipokea timu hiyo katika viwanja vya ndege vya Kimataifa vya Mwalimu Nyerere ambapo Waziri Mwakyembe aliwataka walimu na wachezaji hao kuendelea kujiandaa kwa ajili ya mashindano mengine yaliyo mbele yao.

“Nimefurahi kwa hatua mliyoifikia na watanzani wote wanawapongeza kwa kuwa mmeshindana kwa uwezo wenu na kuirudisha Tanzania katika ramani ya soka baada ya kukaa nje ya michezo ya AFCON kwa takribani miaka 30 alisema” Mhe Mwakyembe.

Aidha aliongeza kuwa hapo walipofika wao ni mashujaa na Serikali inaahidi kushirikiana nao katika kuhakikisha kuwa vipaji hivyo vinaendelezwa kwa ajili ya ngazi nyingine za kisoka.

Naye Kocha wa Serengeti Boys Kim Paulsen ameiomba Serikali na wadau wa michezo nchini kuendelea kuisadia timu hiyo katika maandalizi mbalimbali ili kuipa motisha zaidi katika kufanikisha ndoto ya Tanzania katika mchezo wa soka.

Kwa upande wake kapteni wa timu ya Serengeti Boys Bw. Dickson Job amewashukuru watanzania kwa mchango mkubwa walioutoa kwao katika maandalizi mpaka hapo walipofikia ingawa hawakufanikiwa kurudi na ushindi.

“Mchezo una matokeo matatu kushinda, kushindwa au kutoka sare ingawa hatukutarajia kushindwa kwa kuwa tulitamani sana kurudi na ushindi kama ambavyo tuliwaahidi watanzania ila mwaka huu bahati haikuwa yetu ila tunaahidi kuendeleza mapambano katika hatua zijazo” alisema Bw. Job

Timu ya Serengeti Boys imerejea nyumbani baada ya kumalizika kwa michuano ya AFCON ambapo watapumzika na kuingia kambini kwa ajili ya kujiandaa na michuano inayofuata ya chini ya miaka 20 inayounda timu ya Ngorongoro Heroes.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (kulia) akimpa mkono wa kumkaribisha nyumbani mchezaji wa Serengeti Boys Bw. Abdul Sulemani (kushoto) katika hafla ya kuwapokea wachezaji hao waliorejea nchini kutoka katika michuano ya AFCON nchini Gabon jana Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (katikati waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na wachezaji wa Serengeti Boys pamoja na viongozi wa timu hiyo katika hafla ya kuwakaribisha baada ya kurejea kutoka katika michuano ya AFCON nchini Gabon jana Jijini Dar es Salaam.
Wachezaji wa timu ya vijana chini ya miaka 17 “Serengeti Boys” wakimsikiliza Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (hayupo katika picha) katika hafla ya kuwakaribisha baada ya kurejea kutoka katika michuano ya AFCON nchini Gabon jana Jijini Dar es Salaam. (Picha na: Lorietha Laurence - WHUSM).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...