Mkuu wa Wilaya ya Simanjiro Mkoani Manyara, mhandisi Zephania Chaula (pichani) amewataka wananchi wa Kijiji cha Losoito, kuitunza na kutohujumu
miundombinu ya maji yaliyowezeshwa na kampuni ya TanzaniteOne.
Mhandisi Chaula aliyasema hayo juzi alipofanya ziara ya siku moja
kwenye kijiji hicho baada ya kupatiwa taarifa kuwa kuna baadhi ya
watu wameharibu miundombinu hiyo kwa kukata mabomba.
Alisema miundombinu hiyo imewezeshwa kwa pamoja na kampuni ya
TanzaniteOne na Serikali kwani wanamiliki mgodi huo kwa asilimia 50
kwa 50 hivyo jamii inapaswa kuyatunza kuyathamini na kuyalinda maji.
Alisema atamchukulia hatua mtu yeyote atakayekamatwa akiharibu
miundombinu ya maji kwani wananchi wa eneo hilo kwa muda mrefu
waliteseka kufuata huduma hiyo umbali mrefu hadi Mirerani.
“Nimeambiwa awali kuna mama alishajifungua njiani wakati akifuata maji
na baba wa kimasai akakata kitovu cha mtoto kwa kutumia sime kasha leo
mtu anaharibu miundombinu hii,” alisema mhandisi Chaula.
Mkazi wa Kijiji hicho, Magdalena Peter alisema anashukuru kampuni ya
TanzaniteOne kwa kuwezesha mradi huo wa maji ila bado kuna changamoto
ya upatikanaji kwani wanayapata mara mbili kwa wiki.
“Awali tulikuwa tunapata maji hayo kwa wakati fofauti na tulivyokuwa
tunatembea kilomita 40 hadi Mirerani ila hivi sasa tunawakati mgumu
baada ya tenki hilo kupasuka,” alisema Peter.
Ofisa mahusiano wa kampuni ya TanzaniteOne, Halfan Hayeshi alisema
anaomba apewe muda wa wiki mbili ili ahakikishe anafanyia matengenezo
sehemu za miundombinu iliyoharibika eneo hilo.
“Nitakuja na mafundi wiki ijayo ili waangalie na kuikarabati
miundombinu hiyo na pia tutanunua tenki lenye ujazo wa lita 10,000
tofauti na hili la lita 5,000 linalotumika hivi sasa,” alisema
Hayeshi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...