Na Karama Kenyunko, Globu ya Jamii.
MAPEMA hii leo, upande wa Mashtaka katika kesi inayomkabili raia wa AfriKa Kusini, Menolaos Tsampos, (61), umeileza mahakama kuwa, mshtakiwa huyo hana uhalali wa kuishi nchini ingawa imethibitika kuwa ni kweli ana makazi eneo la mbezi jiji Dar es Salaam.

Wakili wa Serikali Nassoro Katuga amesema hayo mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi, Cyprian Mkeha wa mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu alipokuwa akiwasilisha ripoti ya ya mahakama iliyowaagiza kwenda kukagua makazi ya mshtakiwa pamoja na hati ya mshtakiwa.

Amesema, kamishna wa Uhamiaji nchini amethibitisha kuwa Tsampos, hana uhalali wa kuishi nchini ila Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Mbezi amethibitisha kuwa, mshtakiwa huyo ni kweli anayo makazi ya kuishi eneo hilo.

Hata hivyo, wakili wa utetezi, Jebra Kambole, ameomba mahakama kumpatia dhamana mshtakiwa huyo kwani imedhihirisha kuwa ni kweli mshtakiwa anaishi Mbezi na pia Kamishna wa Uhamiaji hajaeleza ni kwa nini hana uhalali wa kuishi hapa nchini.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi kesho kwa ajili ya kutolewa uamuzi kama apatiwe dhamana au la.

Raia huyo wa Afrika Kusini, anakabiliwa na mashtaka ya kutishia kwa mtandao, kuishi nchini kwa muda wa miaka minne bila kibali na kutumia paspoti yenye visa ya kugushi.
 Raia wa AfriKa Kusini, Menolaos Tsampos, (61) aliyekuwa anashikiliwa kwa makosa manne leo tena amesomewa mashtaka katika Mahakama ya hakimu Mkazi Kisutu, mashtaka yake ikiwemo kuishi nchini bila kibali.  Leo pia  imethibitishwa kuwa Visa yake ya kusafiria si halali na hana uhalali wa kuishi hapa nchini.

 Raia wa AfriKa Kusini, Menolaos Tsampos, (61)akiwa amejificha sura yake katika mahakama ya Kisutu jijini  Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...