MWAZILISHI na mchungaji Mkuu wa kanisa la Moto halisi (Pure Fire miracles Ministries International'), lililopo Tabata Segerea kwa Bibi
,Dk. Enoch Aminu kutoka nchini Ghana amewasili hapa kwaajili ya
kuwaletea siku tatu za huduma ya ujazo wa upako.
Akizungumza
wakati wa hafla fupi ya kumkaribisha hapa nchini mchungaji huyo kutoka
nchini Ghana, Mchungaji Mwenyeji, Innocent Ikechukwu amesema kuwa
wananchi wajitokeze ili kupata maada mbalimbali za ukombozi na
mafanikio.
Amesema huduma zitatolewa kwa siku tatu kuanzia
leo Jumanne saa 11:00 jioni hadi alhamisi ambapo wahapingani kabisa na
muda wa kazi hapa nchini kutokana na muda huo watu wengi watakuwa
wametoka makazini.
Huduma hiyo itatolewa kwa lengo la kusaidia wanachi wenye matatizo mbalimbali, ili kupata upanyaji na kumtumaini Mungu,pamoja na Ukombozi na Mafanikio ambapo wanawaalika watu mbalimbali kuhudhulia mkutano huo ambapo mtoa maada katika siku tatu mfululizo ili kujipatia huduma za ukombozi na mafanikio.
Mkuu
wa Kanisa hilo, Dk. Enoch Aminu kutoka nchini Ghana akizungumza na
waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo mara baada ya kuwasili
katika Kanisa la Moto halisi (Pure Fire miracles Ministries International') lilopo Tabata Segerea kwa Bibi jijini Dar es Salaam.
Mchungaji Mwenyeji, Innocent Ikechukwuakizungumza wakati wa kumkaribisha Mkuu wa Kanisa hilo, Dk. Enoch Aminu kutoka nchini Ghana mara baada alipo wasili kanisani hapo jijinio Dar es Salaam leo.
Pia
amemshukuru kwa kuitikia wito wake kuja hapa nchini kutoa huduma ya
neno la Mungu pamoja na ukombozi wa Mafanikio ya wanajamii watakao
hudhuria katika huduma kanisani hapo.
Baadhi ya waumini wa Kanisa la Moto halisi (Pure Fire miracles Ministries International') lilopo Tabata Segerea kwa Bibi wakimuaga Mkuu wa Kanisa hilo, Dk. Enoch Aminu kutoka nchini Ghana mara baada ya kufika na kuongea na waumini hao.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...