Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Dkt. Adelhelm Meru (watatu kutoka kulia) akikata utepe katika ufunguzi wa Duka la vifaa vya Ujenzi la Jotun Tanzania, lililopo Mtaa wa Mkwepu, Posta Mpya jijini Dar es salaam. Kushoto kwake ni Balozi wa Norway nchini, Bi. Hanne Marie Kaarstad na wa pili kushoto ni Makamu Rais wa JOTUN, Esben Hersve. Kampuni ya Jotun iliyoanzishwa nchini Norway mwaka 1926, ni moja ya kampuni zinazoongoza katika uzalishaji wa rangi duniani, ambapo mwaka 1974 Jotun waliweka uwepo wao katika nchi za umoja wa nchi za kiarabu, tangu wakati huo Jotun imekuwa ikikuwa katika maeneo tofauti, na kuwa kampuni pekee ya uzalishaji rangi  iliyopata tunzo ya vyeti vya viwango vya ubora vyenye  namba  ISO 9001: 2008, ISO 14001 & OHSAS 18001. Kampuni hii pia ina viwanda vya uzalishaji katika nchi ya Abu Dhabi, Dubai, Saudi Arabia, Oman na Misri.
Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji Dr. Adelhelm Meru, akipewa maelekezo ya namna mashine ya uchanganyaji rangi inavyofanya kazi toufauti kwa dakika moja.
Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji Dr. Adelhelm Meru, akihutubia katika sherehe za ufunguzi wa duka la rangi ya Jotun Tanzania.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...