Na Omary Mngindo, Kibaha

MKUU wa Wilaya ya Kibaha Mkoa wa Pwani Bi. Assumpter Mshama amemaliza mgongano wa Wafanyabiashara wenye ubao upande wa ndani na wanaouzia kandokando ya Barabara.

Mgongano huo uliokuwepo kwenye soko la Mnalani Maarufu Loliondo kati ya Wafanyabiashara hao ambapo wanaouza ndani kwenye mbao wanadai wateja wanaishia nje hivyo hawapati wateja.

Wafanyabiashara Godruck Mwafrika na Anelista Mbaga kila mmoja amwelezea changamoto iloyopo kwenye soko hilo hali inayoleta mgongano kati yao.Mwafrika alisema kuwa waliowengi wamekimbia meza za ndani na kwenda kupanga nje kwa lengo la kupata wateja kwani wengi wanaishia nje hivyo wao kubaki wakipunga upepo tu.

Kauli hiyo ilipingwa na Bi. Aneliata ambaye alisema wote wanafanyabiashara sawa na kwamba malalamiko hayo hayana msingi huku akisema kwamba wateja wanafika kununua bidhaa sawasawa.

Baada ya kupata malalamiko ya pande mbili, Mshama ameagiza wanaofanyia biashara pembeni mwa soko wote waingie ndani na kwamba meza zote zina upana wa mita 30 hivyo kila moja watakaa watu wawili kwa maana mita 15.

Aidha amevunja aoko la siku za Jumatano akisema hatua hiyo ni ya ujanja wa watu ambapo alisema zuio hilo litaanzia Jumatano ya wiki inayoanzia Oktoba 25 akieleza kwa kiwa agizo hilo limekujanghafla kwani wapomm watu ambao wapo maeneo mbalimbali kutafuta biashara.
 MKUU wa Wilaya ya Kibaha Mkoa wa Pwani Bi. Assumpter Mshama akizungumza na Wafanyabashara wa soko la Loliondo.
 Baadhi ya Wafanyabiashara wa soko la Loliondo wakifurahia mara baada ya mgogoro wao kutatuliwa na MKUU wa Wilaya ya Kibaha Mkoa wa Pwani Bi. Assumpter Mshama.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...