NA K-VIS BLOG/KHALFAN SAID.
Mkurugenzi
Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Bw. Adam Mayingu, amewapongeza
wafanyakazi wa Mfuko huo, kwa kazi nzuri wanayofanya ya kuwatumikia
wateja, (wanachama) wa Mfuko.
Bw.
Mayingu ameyasema hayo wakati wa hafla fupi ya kuwatunuku tuzo na
zawadi wafanyakazi waliofanya vizuri zaidi katika kipindi cha Wiki ya
Huduma kwa Wateja, iliyoanza Oktoba 2 na kumalizika Oktoba 6, 2017.
Wiki
hiyo ambayo huadhimishwa kila mwanzo wa wiki ya mwezi Oktoba kila
mwaka, hulenga kuwakumbusha wafanyakazi wajibu wao wa kuwahudumia wateja
kwa kuzingatia weledi wa utoaji huduma bora kwa mteja.
"Wakati
nikiwa Iringa nimepokea pongezi nyingi za Wanachama wetu, wakiwapongeza
nyinyi wafanyakazi kwa kuwahudumia vizuri, hongereni sana na niwaombe
muendele kutoa huduma bora kwa wateja wetu kwani huo ndio wajibu wetu."
Alisema Bw. Mayingu katika hafla hiyo iliyofanyika Oktoba 6, 2017 kwenye
ukumbi wa makao makuu ya PSPF, Jubilee Tower jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi
Mkuu wa PSPF, Bw. Adam Mayingu, akiwahutubia wafanyakazi na wadau wa
Mfuko, wakati wa hafla ya kuwatunuku tuzo na kuwakabidhi zawadi
wafanyakazi "waliochomoza" kwa utoaji huduma bora zaidi katika kipindi
cha Wiki ya Huduma kwa Wateja, 2017, iliyofikia kilele Oktoba 6, 2017.
Bw. Mayingu akimkabidhi tuzo, Elizabeth Shayo.
Bw. Mayingu akimkabidhi tuzo, Bi.Valley Malinga
Meneja wa Mpango wa Uchangiaji wa Hiari, (PSS), Bi. Mwanjaa Sembe, (wapili kushoto), akiwa na maafisa waandamizi wa Mfuko huo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...