Mbunge wa Songea mjini na Diwani wa Songea mjini, mkoa wa Ruvuma, Mhe. Leonidas Gama Enzi za uhai wake akiwa kwenye kikao cha madiwani. Mhe. Gama amefariki usiku wa kuamkia leo Novemba 24, 2017, wakati akipatiwa matibabu kwenye hospitali ya Peramiho mkoani humo. Itakumbukwa ya kwamba Mhe. Gama alikuwa nchini India ambako nako alikuwa akitibiwa. 

Mheshimiwa Gama kabla ya kuwa mbunge amewahi kushika nyadhifa nyingine za kiserikali ikiwemo Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro wakati wa utawala wa awamu ya Nne. Bunge limethibitisha ,kutokea kwa kigfo hicho na kwamba taarifa Zaidi zoitatolewa baadaye. 

Taarifa za kifo chake zimeanza kusambaa kwenye mitandao ya kijamii ambapo marafiki zake wa karibu na marehemu, akiwemo diwani wa Mwananyamala jijini Dar es Salaam, Mhe. Songoro Mnyonge ameandika katika ukurasa wake wa Facebook, akieleza kusikitishwa kwake na kwamba taarifa za kifo cha mbunge huyo amezipokea majira ya saa 7 usiku wa kuamkia leo Novemba 24, 2017.

Katika maandishi yake Mhe. Mnyonge alieleza masikitiko yake kwani ni wiki tatu tu Mhe. Gama alimpigia simu Mhe. Songoro Mnyonge na walijadiliana kuhusu matibabu ya nduguye, Dominic Gama ambaye anapatiwa matibabu nchini Afrika Kusini.
Mbunge wa Jimbo la Songea Mjini, Leonidas Gama akipimwa afya na Muuguzi Asha Shao bungeni Dodoma.
Katika picha hii ya maktaba, Rais mstaafu wa awamu ya nne, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, akimuapisha Mhe. Leonidas Gama kuwa Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro.
Katika picha hii ya maktaba Mhe. Waziri Mkuu, akizungum,za jambo na Mhe. Leonidas Gama, mbunge wa Songea mjini, kwenye viwanja vya bunge mjini Dodoma.
Katika picha hii ya maktaba, Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Mhe.Leonidas Gama akisalimiana na viongozi wa wilaya ya Rombo mara baada ya kuwasili katika shule ya sekondari Olele kwa ziara ya kikazi.
Mhe. Gama (mwenye jaketi jeupe), akiwa na viongozi wengine wa mkoa wa Kilimanjaro, akitekeleza majukumu yake Enzi za uhai wake.
Mhe. Leonidas Gama akiwa na wabunge wenzake, Mhe. Hamisi Kigwangalla, (mbunge wa Nzega), na Mhe. Sixtus Mapunda, Mbunge wa Mbinga mjini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...