Mkurugenzi Mtendaji was hospital ya rufaa ya Mbeya Dr Godlove Mbwanji akitoa shurkani kwa Mkuu wa Kitengo cha Masoko na mawasiliano wa Benki ya Exim Tanzania, Stanley Kafu (kushoto) baada ya kukabidhiwa msaada wa vitanda na magodoro 40 kutoka benki hiyo jana asubuhi kwa ajili ya wagonjwa katika hospitali hiyo kitengo cha wazazi-Mbeya jijini Mbeya.  Wa pili kulia ni Mkuu wa idara ya wodi ya wazazi-Meta, katika hospitali hiyo Dr John France.

HOSPITALI na kliniki nyingi nchini zina tatizo la ukosefu wa dawa, vifaa na vitanda hasa katika hospitali za rufaa.  Katika kukabiliana na uhaba huu unaosumbua taifa , Exim Bank Tanzania, yenye uwepo wa kimataifa  imeanzisha mradi unaolenga kusaidia upungufu wa vitanda katika hospitali nchini - hivyo benki ya Exim itatoa magodoro and vitanda 500 katika hospitali za serikali katika mikoa 13 nchini kama sehemu ya kampeni yake yenye lengo la kusherehekea miaka 20 ya kutumikia jamii.

Benki ya Exim Tanzania iliadhimisha miaka 20 ya huduma, mwezi wa Agosti mwaka jana, kwa kuzindua mradi wa mwaka mzima unaoitwa “miaka 20 ya kujali jamii” ambao Benki hiyo itawekeza katika sekta ya afya Tanzania. Kama benki ya kiTanzania iliyoanzishwa mwaka wa 1997, Benki ya Exim inafafanua mafanikio kwa jinsi inavyoleta mabadiliko kwa wateja na jamii kwa ujumla.

Hospitali ya rufaa ya mkoa wa Mbeya, ni hospitali ya sita kupokea mchango huu, baada ya Hospitali ya Mkoa ya Mount Meru, Arusha mwezi uliopita, Hospital ya rufaa Dodoma mwezi Novemba, hospitali ya rufaa Ligula, Mtwara mwezi Oktoba, Hospitali ya Mnazi Mmoja, Unguja, Zanzibar mwezi Septemba na Hospitali ya rufaa Temeke, Dar es Salaam mwezi wa nane mwaka jana. Tukio lilifanyika kwenye hospitali hiyo wodi ya wazazi META na mgeni rasmi alikuwa Mkurugenzi mtendaji wa hospitali hiyo Dr. Godlove Mbwanji.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...