Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi amesema kuwa wafanyakazi wa SMZ wataongezewa posho ya shilingi 50,000 ya nauli ili kuleta ufanisi katika kazi na kurahisisha masuala ya usafiri kwa ajili ya nauli za kwenda kazini na kurudi nyumbani.

Amesema shilingi bilioni 34 zimetengwa na Serikali kwa ajili ya posho ya usafiri kwa watumishi wote wanaostahiki kulipwa posho.

Rais Dk.Mwinyi amesema hayo katika sherehe za Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi duniani (Mei Mosi) zilizofanyika uwanja wa Gombani, Mkoa wa Kusini Pemba tarehe 1 Mei 2024.

Aidha Rais Dk.Mwinyi amesema Serikali imejipanga kutengeneza ajira 300,000 kwa wananchi wake kwa mujibu wa Ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020-2025.

Halikadhalika Rais Dk.Mwinyi ameeleza kuwa katika kipindi cha miaka mitatu Serikali kupitia shughuli utekelezaji wa miradi ya maendeleo ajira mpya zipatazo 187,651 zimepatikana sawa na asilimia 104 ya lengo la ajira 180,000 kwa miaka mitatu iliyopita.

Kwa upande mwingine Rais Dk.Mwinyi amesema Serikali imedhamiria kuhakikisha inaongeza fedha kwa ajili ya posho ya likizo , zikiwa zimetengwa shilingi bilioni 2.5 katika bajeti mpya ya mwaka 2024/25.







  

Na. Vero Ignatus Arusha

Maadhimisho ya sherehe za mei mosi kit aifa yamefanyika Mkoani Arusha ambapo yamekuwa na zaidi ya waandamanaji 7000 mbali na wananchi ambao walioshiriki katika maadhimisho hayo.

Akitoa salam za mkoa mkuu mkoa wa Arusha Paul Christian Makonda aliweza kumuomba Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Mpango kufikisha salamu kwa Rais wa Dkt. Samia Suluhu Hassan wakazi wa Arusha wanatambua mchango wake hasa kwenye sekta ya utalii.

"Wananchi wa jiji la Arusha na mkoa wa Arusha kwa ujumla wake wanayo furaha kubwa sana kwa kazi kubwa aliyoifanya ya 'Royal Tour' na hivi tunaelekea kwenye high season hivyo tunategemea kupata watalii wengi sana, na kwetu sisi wananchi wa kila kada awe ni muuza mchicha, awe ni Bodaboda, awe ni mtu anayelima nyanya, Bilinganya nk anafaidika na utalii kwa kuwa Hoteli zikijaa na yeye anapata nafasi ya kuuza na hatimaye anaendesha maisha yake" Alisema Makonda

Sambamba na salam hizo Makonda aliweza kutoa ombi lake kwa mgeni Rasmi kwamba Rais kwamba jiji hilo Lina mchango makubwa wa wadau wa utalii, hivyo ameomba kusaidiwa kutengeneza barabara ya Jiji hilo,kwani barabara siyo nzuri na wananchi wanashindwa kufanya kazi zao kwa usahihi, lna kwa usalama

"Tunataka kufanya utalii wa Jiji letu kwa lands nzima ya kaskazini tumekubaliana kuanzisha kituo ki moja cha uwekezaji (one stop Center) Jiji la Arusha."

Makamu wa Rais Dkt Philip Isdory Mpango akijibu risala ya TUCTA alisema kuwa kuhusu nyongeza ya mishahara mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali ilipandisha kima cha chini cha mishahara kwa asilimia 23.3 kutoka shilingi 300,000 (laki tatu) hadi shilingi 370,000 kwa mwezi, lengo la kutoa nyongeza kwa kiwango hicho ilikuwa ni kuwezesha watumishi wenye mishahara ya kima cha chini kumudu gharama za maisha kwa kadri inavyowezekana

Dkt Mpango amesema makundi mengine ya watumishi ambayo yaliguswa na ongezeko hilo la mishahara kwa viwango tofauti kwa kuzingatia ukomo wa bajeti wa mishahara iliyotengwa, huku akiendelea kusema kuwa serikali itaendelea kuhuisha viwango vya mishahara kwa kuzingatia uwezo wa kiuchumi na kibajeti pamoja na ujuzi na utendaji wa waajiriwa, misingi hii ni muhimu ili kuepuka kuchochea mfumuko wa bei kuhatarisha uhimilivu wa deni la Taifa na athari nyingine kwenye uchumi wa Taifa kwa ujumla.

"Haya yote lazima yazingatiwe katika mchakato wa kuongeza mishahara na hususani katika kipindi ambapo uchumi wa Dunia umekumbwa na misukosuko mingi ikiwemo vita baina ya Urusi na Ukraine, vita vya mashariki ya kati inayohusisha Israel, Palestina, Lebanon, Syrian, Iran na Yemen" Alisema Dkt. Mpango

Dkt. Mpango. Amesema Vita hivyo vimepelekea kuvurugika kwa mfumo wa ugavi na kupanda sana kwa bei ya mafuta, mbolea, chuma na chakula, na kama hiyo haitoshi Dunia imekumbwa na majanga mengine ikiwemo mvua kubwa na maporomoko ya udongo ambayo yamesababisha uharibifu mkubwa wa miundombinu, magonjwa na hata vifo.

"Changamoto zote hizi zimeathiri pia uchumi wetu, hivyo Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan mama wa Taifa ameniagiza niwaambie wafanyakazi wa Tanzania kuwa endapo hali hii itadumu wafanyakazi wawe na matumaini kwamba atasema jambo hivi karibuni" -Dkt. Mpango

Kawa upande wake Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Kassim Majaliwa amewapongeza wakazi wa Mkoa wa Arusha kwa hamasa na maandalizi ya sherehe za Siku ya Wafanyakazi Duniani leo Mei Mosi, 2024.

Aidha ameahidi kuwa Ofisi Yake itaendelea kishriikiana na vyama hya wafanyakazi kuangalia namna gani wanaweza kutatua changamoto mbakimbali zitakazojitokea.






Mwamvua Mwinyi, Kibaha
Mei 1

MWENGE wa Uhuru utapitia miradi 28 yenye thamani ya trilioni 8.5 wilayani Kibaha, mkoani Pwani, ambapo umekagua mradi mkubwa wa
Kongani ya Viwanda ya SINOTAN, Kata ya Kwala ambao hadi kukamilika utagharimu trilioni 8.4.

Aidha umeweka jiwe la msingi mradi wa ujenzi wa barabara kutoka barabara ya Morogoro kwenda ofisi za Halmashauri, yenye urefu wa mita 300 kiwango cha lami , thamani mil490,018,125 fedha za ujenzi kutoka Serikali Kuu -Maendeleo ya Jimbo.

Akitoa taarifa kwa Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava, Meneja wa TARURA wilayani Kibaha, Samwel Ndoveni alisema, mradi umetekelezwa na Mkandarasi M/S Globalink General Contractors Ltd.

Nae Mzava ameridhishwa na mradi huo wa barabara,na kusisitiza umuhimu wa manunuzi ya umma kupitia katika mfumo wa kidigital wa manunuzi ya umma Nest ambao unasimamiwa na mamlaka ya udhibiti ya manunuzi ya umma (PPRA).


Alieleza mfumo huo, unasaidia kuondoa tabia iliyokuwa ikijitokeza kipindi cha mfumo wa zamani TANREP.


Mzava alifafanua,mfumo huo umeondoa malalamiko ,na tabia za watu kukutana mezani na kupeana zabuni.


"Zamani tulikuwa na mfumo wa TANREP na sasa tuna mfumo wa NEST na waheshimiwa wabunge wametutungia sheria nzuri ya kusimamia mambo hayo na ndio maagizo ya Rais Samia Suluhu Hassan ili kupunguza malalamiko na kuweka udhibiti katika matumizi ya umma "alisema Mzava.


Katika hatua nyingine, Mwenge wa Uhuru uliweka jiwe la uzinduzi wa mradi wa maji kijiji cha Ruvu Stesheni, kumtua mama ndoo kichwani ,mradi ambao unasimamiwa na Mamlaka ya maji safi Na mazingira Vijijini (RUWASA) .


Deborah Kanyika Meneja RUWASA Kibaha, alielezea chanzo cha mradi huo ni kisima chenye uwezo wa kutoa lita 11,820 kwa saa na kina urefu wa mita 43 , gharama za mradi 328,719,109.94 kupitia mfuko wa Taifa wa maji (NWF) .


Deborah alisema,kabla ya kujengwa mradi huo kaya 81 zilikuwa zinapata maji kwasasa kaya 164 zinakwenda kunufaika kati ya hizo 33 zimeunganishiwa maji nyumbani, mradi huo umesanifiwa kuweza kutoa huduma hadi kufikia kaya 520 ifikapo 2042.


Mwenge huo pia umekagua na kufungua mradi wa ujenzi wa vyumba vitatu vya madarasa na matundu matano ya vyoo shule ya msingi Kilangalanga na kituo cha wanafunzi wenye mahitaji maalum shule ya msingi Mlandizi.


Awali akipokea Mwenge wa Uhuru kutoka Bagamoyo, Mkuu wa wilaya ya Kibaha, Nikkison John alisema, Mwenge huo utapitia miradi 28 katika halmashauri ya Kibaha Mjini na Kibaha Vijijini ,yenye thamani ya trilioni 8.5.







Gwaride la Heshima la Vijana wa kujitolea likipita mbele ya Mkuu wa Wilaya ya Kigoma, Salum Kalli (hayupo pichani) kabla ya kufunga mafunzo ya awali ya kijeshi kwa vijana wa Kujitolea 'Operesheni ya Miaka 60 ya JKT', katika kikosi cha Jeshi cha 821, Bulombora,hafla iliyofanyika Mkoani Kigoma.

Na.Alex Sonna-KIGOMA

MKUU wa Wilaya ya Kigoma, Salum Kalli amewataka vijana waliopata mafunzo ya awali Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kujiepusha na matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii yaliyo kinyume na mila na utamaduni wa Watanzania.


Mhe.Kalli ameyasema hayo Mkoani Kigoma wakati akifunga mafunzo ya awali ya kijeshi kwa vijana wa Kujitolea 'Operesheni ya Miaka 60 ya JKT', katika kikosi cha Jeshi cha 821, Bulombora.

Mhe.Kalli,amewaonya juu ya matumizi ya mitandao ya jamii yanayotokana na ukuaji wa teknolojia ambayo yamemfanya kila Mtanzania kutamani kutumia simu janja ambazo zimekuwa na mambo mengi kiasi cha mtu kufahamu kila kinachofanyika duniani kupitia mitandao ya kijamii.

“Vijana wengi wamekuwa hawana elimu ya kutosha juu ya matumizi sahihi ya mitandao ya kijamii, hivyo basi hutazama mambo ambayo ni kinyume kabisa na tamaduni zetu za kiafrika. Ninawaomba sana msiingie huko kwenye mitego isiyo yenu, hakikisheni mnalilinda Taifa lenu,”amesema Mhe.Kalli

Aidha amewataka kuhakikisha wanalinda Taifa, wanasimamia miongozo, uadilifu na maelekezo ya kila siku ili nchi iendelee kuwa salama.

Pia amesema kuwa Serikali ilitunga Sheria ya Kudhibiti Maudhui Mtandaoni ambapo watakapopatikana na maudhui ambayo ni kinyume na mila na utamaduni, hatua kali za sheria zitacjhukuliwa dhidi yao.

“Natumia fursa hii kuwaasa kuwa hatutakuwa na wasaa mwingine tutakapokuta wewe umeingia kwenye makundi yasiyofaa ambayo siyo yale uliofundishwa hapa (jeshini) ukaingia katika mitandao ya hatakuwa na saa nyingine ya kutoa wasia wakati watakapofanya mambo ya hovyo, bali watawachukulia hatua za kisheria mara moja,”amesema. Aidha, amewataka kusimamia nchi yao kuwa wazalendo, waadilifu na kutokubali nchi yao ikalindwa na watu wengine na badala yake kulinda wenyewe kwa utii waliofundishwa lakini wakisimamia kiapo chao na miongozo na maelekezo ya Amiri Jeshi Mkuu Dk Samia Suluhu Hassan.

Mhe.Kalli ameipongeza Serikali chini ya Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuwezesha ufanyikaji wa mafunzo hayo ambayo ni muhimu kwa ustawi wa Vijana wetu na Taifa kwa ujumla. "Nipende kulishukuru Jeshi la Kujenga Taifa na Watendaji wote chini ya uongozi Shupavu wa Meja Jenerali Rajabu Nduku Mabele kwa kusimamia kwa weledi mkubwa malezi ya vijana wetu na hatimaye kufikia viwango bora."

Kwa upande wake Mwakilishi wa Mkuu wa JKT, Meja Jenerali Rajabu Mabele, Mkuu wa Tawi la Utawala JKT, Brigedia Jenerali Hassan Mabena amesema mafunzo hayo ni mwendelezo wa utekelezaji mawazo ya muasisi wa Taifa, Baba wa taifa hayati Mwalimu Julius Nyerere katika uanzishwaji wa JKT.

”Naamini kuwa mafunzo haya mliyoyapata mmekuwa tayari kulitumikia na kulilinda taifa letu popote mtakapokuwa kwani mmefahamu dhana ya uzalendo, umoja, mshikamano, ukakamavu na kujiami, mnapaswa kutumia elimu hii katika kutatua changamoto mbalimbali pasipo kuvunja sheria na taratibu za nchi. Hivyo nendeni mkaishi kiapo chenu.”amesema Brigedia Jenerali Mabena

Aidha Brigedia Jenerali Mabena amewataka vijana hao kutunza afya zao kwani ndio msingi na mtaji wao mkubwa na kujiepusha na vitendo vya uvunjifu wa amani, ulevi, utumiaji wa dawa za kulevya, ulaji wa vyakula au utumiaji wa vinywaji vyenye kuhatarisha afya zao.

Awali, Kamanda Kikosi cha 821 KJ Bulombora, Luteni Kanali Juma Hongo, amesema mafunzo ya vijana wa kijitolea Operesheni miaka 60 ya Jeshi la Kujenga Taifa yalianza Desemba 2023 na kufanyika kwa majuma 16 mfululizo ambapo vijana wamejifunza mambo mbalimbali ikiwemo mbinu za kivita, ujanja wa porini, usomaji wa ramani, usalama na utambuzi kukabliana na majanga na matumizi ya silaha ndogondogo, kazi za mikono na uzalishaji mali kwa vitendo.

”Lengo likiwa ni kukuza moyo wakizalendo, kuwajengea ukakamavu, ujasiri, uwezo wa kutumia muda vizuri kwa kufanyakazi na pia wajitambue kuwa wao ni sehemu ya jamii ya watanzania wanaopaswa kupata mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa.”amesema Luteni Kanali Hongo


MKUU wa Wilaya ya Kigoma, Salum Kalli,akikagua Gwaride la Heshima kabla ya kufunga mafunzo ya awali ya kijeshi kwa vijana wa Kujitolea 'Operesheni ya Miaka 60 ya JKT', katika kikosi cha Jeshi cha 821, Bulombora,hafla iliyofanyika Mkoani Kigoma.


Gwaride la Heshima la Vijana wa kujitolea likipita mbele ya Mkuu wa Wilaya ya Kigoma, Salum Kalli (hayupo pichani) kabla ya kufunga mafunzo ya awali ya kijeshi kwa vijana wa Kujitolea 'Operesheni ya Miaka 60 ya JKT', katika kikosi cha Jeshi cha 821, Bulombora,hafla iliyofanyika Mkoani Kigoma.


MKUU wa Wilaya ya Kigoma, Salum Kalli,akizungumza wakati akifunga mafunzo ya awali ya kijeshi kwa vijana wa Kujitolea 'Operesheni ya Miaka 60 ya JKT', katika kikosi cha Jeshi cha 821, Bulombora,hafla iliyofanyika Mkoani Kigoma.



Kamanda Brigedi 202,Brigedia Jenerali Gabriel Kwiligwa,akizungumza wakati wa hafla ya kufunga mafunzo ya awali ya kijeshi kwa vijana wa Kujitolea 'Operesheni ya Miaka 60 ya JKT', katika kikosi cha Jeshi cha 821, Bulombora,Mkoani Kigoma.



Mwakilishi wa Mkuu wa JKT, Meja Jenerali Rajabu Mabele, Mkuu wa Tawi la Utawala JKT, Brigedia Jenerali Hassan Mabena,akizungumza wakati wa hafla ya kufunga mafunzo ya awali ya kijeshi kwa vijana wa Kujitolea 'Operesheni ya Miaka 60 ya JKT', katika kikosi cha Jeshi cha 821, Bulombora,Mkoani Kigoma.



Kamanda Kikosi cha 821 KJ Bulombora, Luteni Kanali Juma Hongo,akizungumza wakati wa hafla ya kufunga mafunzo ya awali ya kijeshi kwa vijana wa Kujitolea 'Operesheni ya Miaka 60 ya JKT', katika kikosi cha Jeshi cha 821, Bulombora,Mkoani Kigoma.



Baadhi ya Wananchi wakifatilia matukio mbalimbali wakati wa hafla ya kufunga mafunzo ya awali ya kijeshi kwa vijana wa Kujitolea 'Operesheni ya Miaka 60 ya JKT', katika kikosi cha Jeshi cha 821, Bulombora,Mkoani Kigoma.



Vijana wa JKT wakionyesho ufundi wao kwa mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya ya Kigoma, Salum Kalli,(hayupo pichani) wakati wa hafla ya kufunga mafunzo ya awali ya kijeshi kwa vijana wa Kujitolea 'Operesheni ya Miaka 60 ya JKT', katika kikosi cha Jeshi cha 821, Bulombora,Mkoani Kigoma.
Mwamvua Mwinyi, Kibaha
Mei 1

MWENGE wa Uhuru utapitia miradi 28 yenye thamani ya trilioni 8.5 wilayani Kibaha, mkoani Pwani, ambapo umekagua mradi mkubwa wa
Kongani ya Viwanda ya SINOTAN, Kata ya Kwala ambao hadi kukamilika utagharimu trilioni 8.4.

Aidha umeweka jiwe la msingi mradi wa ujenzi wa barabara kutoka barabara ya Morogoro kwenda ofisi za Halmashauri, yenye urefu wa mita 300 kiwango cha lami , thamani mil490,018,125 fedha za ujenzi kutoka Serikali Kuu -Maendeleo ya Jimbo.

Akitoa taarifa kwa Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava, Meneja wa TARURA wilayani Kibaha, Samwel Ndoveni alisema, mradi umetekelezwa na Mkandarasi M/S Globalink General Contractors Ltd.

Nae Mzava ameridhishwa na mradi huo wa barabara,na kusisitiza umuhimu wa manunuzi ya umma kutumia mfumo wa kidigital wa manunuzi ya umma Nest ambao unasimamiwa na mamlaka ya udhibiti ya manunuzi ya umma (PPRA).

Alieleza mfumo huo, unasaidia kuondoa tabia iliyokuwa ikijitokeza kipindi cha mfumo wa zamani TANREP.

Mzava alifafanua,mfumo huo umeondoa malalamiko ,na tabia za watu kukutana mezani na kupeana zabuni.


"Zamani tulikuwa na mfumo wa TANREP na sasa tuna mfumo wa NEST na waheshimiwa wabunge wametutungia sheria nzuri ya kusimamia mambo hayo na ndio maagizo ya Rais Samia Suluhu Hassan ili kupunguza malalamiko na kuweka udhibiti katika matumizi ya umma "alisema Mzava.


Katika hatua nyingine, Mwenge wa Uhuru uliweka jiwe la uzinduzi wa mradi wa maji kijiji cha Ruvu Stesheni, kumtua mama ndoo kichwani ,mradi ambao unasimamiwa na Mamlaka ya maji safi Na mazingira Vijijini (RUWASA) .


Deborah Kanyika Meneja RUWASA Kibaha, alielezea chanzo cha mradi huo ni kisima chenye uwezo wa kutoa lita 11,820 kwa saa na kina urefu wa mita 43 , gharama za mradi 328,719,109.94 kupitia mfuko wa Taifa wa maji (NWF) .


Deborah alisema,kabla ya kujengwa mradi huo kaya 81 zilikuwa zinapata maji kwasasa kaya 164 zinakwenda kunufaika kati ya hizo 33 zimeunganishiwa maji nyumbani, mradi huo umesanifiwa kuweza kutoa huduma hadi kufikia kaya 520 ifikapo 2042.


Mwenge huo pia umekagua na kufungua mradi wa ujenzi wa vyumba vitatu vya madarasa na matundu matano ya vyoo shule ya msingi Kilangalanga na kituo cha wanafunzi wenye mahitaji maalum shule ya msingi Mlandizi.


Awali akipokea Mwenge wa Uhuru kutoka Bagamoyo, Mkuu wa wilaya ya Kibaha, Nikkison John alisema, Mwenge huo utapitia miradi 28 katika halmashauri ya Kibaha Mjini na Kibaha Vijijini ,yenye thamani ya trilioni 8.5.



Njombe

Wananchi wa mtaa wa Muungano halmashauri ya mji wa Makambako mkoani Njombe wamegomea kuuzika mwili wa kijana Elisha Nyalusi (35) wakidai kifo chake kimesababishwa na imani za kishirikina huku wakimtuhumu baba yake na kutaka arudishwe akiwa hai.

Wananchi hao akiwemo Nickson Nywage,Eliud Mwenda na Salima Mangula wamesema wamegomea kuuzika mwili huo kutokana na vijana wenzao wengine watatu kupoteza maisha katika mazingira ya kutatanisha na kueleza kuwa vifo vyao vyote vimetokea tarehe za mwisho wa mwezi.

"Nadhani kulikuwa na mzozano wa shamba baadaye baba yake akamtuma akanunue dawa (roud up) ndipo alipodoka likimsokota tumbo kwa hiyo tumesusia kwasababu tumeumia yani sasa mwaka huu wametoka vijana wanne tayari kwa hiyo haturidhiki tunataka amrudishe tunaona vijana wenye nguvu wanapotea"wamesema wananchini

Hata Hivyo Baba wa kijana huyo aliyepoteza  maisha mwenye umri wa miaka 72  amekana kujihusisha na  Masuala ya imani za kishirikina na kueleza kuwa hakuwa na mgogoro wowote na mtoto wake kwani  na ndiye aliyekuwa akimtunza.

"Mtoto wangu tulishamalizana na alinunua shamba kwangu mbele ya mwenyekiti na shamba nilimkabidhi kwa hiyo tulikuwa hatuna changamoto yeyote na huyu mtoto wangu ndio aliyekuwa ananitunza"amesema baba Mzazi

Mwenyekiti wa mtaa wa Muungano Amelye Mteleke amekiri wananchi kugomea kuuzika mwili wa kijana huyo ambapo amesema tayari baba mzazi wa kijana huyo amechukuliwa na Polisi kwa ajili ya usalama wake.

"Inaonekana kuna maneno ya uchochezi yanayoashiria ushirikina amekuwa akiyatamka kwa hiyo vijana wote pamoja na wazee wamekasilishwa wakasema sasa we mzee utazika mwenyewe na familia yake inamtuhumu kwamba ni mshirikina"amesema Mteleke.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, amewataka wakandarasi wazawa waliopewa dhamana ya ujenzi wa Miradi ya umwagiliji kuhakikisha waaitekelza kwa weledi na ubora wa hali ya Kuu.

Majaliwa Ameyasema hayo Jana katika hafla ya utiaji saini mikataba ya ujenzi wa Miradi ya umwagiliaji katika maeneo mbalimbali, iliyofanyika jijini Dodoma.

"Ndugu washiriki nimefurahishwa kuona kuwa asilimia 82 ya wanaokwenda kujenga miradi hii ni wataalamu na hizi ni fursa za ajira kwa Watanzania, lakini ni fursa ya kuongeza ujuzi kupitia miradi hii, vilevile inakwenda kuongeza kipato kwa Watanzania.

"Nitoke rai kwa wakandarasi wazawa, kwanza mbadilike, mnathaani kubwa mmepewa ya kutekeleza miradi na hili ndicho kilio kikubwa cha private seckta (sekta binafsi) leo mmeona serikali imeendelea kutekeleza kwa kuwapa miradi.

"Mjipange vizuri tumieni fursa hii kuihakikishia serikali kwamba mnaweza, lakini nyie mna dhamira zenu kufungua kampuni za ukenzi, mna hiyo dhamira simamieni dhamira zenu. Sisi tunakutegemeeni nyie kufua milango ya ajira.



Kamishna Msaidizi wa Idara ya Usimamizi wa Madeni Wizara ya Fedha, Bw. Omary Khama (wa pili kushoto mstari wa pili) na Kamishna wa Kitengo cha Ubia kati ya Sekta ya Umma na Binafsi wa Wizara ya Fedha, Bw. Bashiru Hussein (kushoto) wakiwa katika maandamano ya wafanyakazi wa Wizara hiyo wakati wa Sherehe za Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani, yaliyofanyika kwa ngazi ya Mkoa katika Viwanja vya Jamhuri, jijini Dodoma yakiwa na kaulimbiu ya “Nyongeza ya Mishahara ni Msingi wa Mafao Bora na Kinga Dhidi ya Hali Ngumu ya Maisha”

Kamishna Msaidizi wa Idara ya Uendelezaji Sekta ya Fedha, Wizara ya Fedha, Bi. Dionesia Mjema, (katikati) akiongoza maandamano ya watumishi wa Wizara hiyo wakati wa Sherehe za Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani, yaliyofanyika kwa ngazi ya Mkoa katika Viwanja vya Jamhuri, jijini Dodoma, yakiwa na kaulimbiu ya “Nyongeza ya mishahara ni Msingi wa Mafao Bora na Kinga Dhidi ya Hali Ngumu ya Maisha”

Watumishi wa Wizara ya Fedha wakipita kwa bashasha mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Bi. Rosemary Senyamule, ambaye alikuwa mgeni rasmi wa Sherehe za Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani, yaliyofanyika kwa ngazi ya Mkoa katika Viwanja vya Jamhuri, jijini Dodoma, yakiwa na kaulimbiu ya “Nyongeza ya mishahara ni Msingi wa Mafao Bora na Kinga Dhidi ya Hali Ngumu ya Maisha”

Kamishna Msaidizi wa Idara ya Sera Wizara ya Fedha, Bw. Mbayan Saruni (katikati) akiteta jambo na baadhi ya watumishi walioshiriki Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani, yaliyofanyika kwa ngazi ya Mkoa katika Viwanja vya Jamhuri, jijini Dodoma, yakiwa na kaulimbiu ya “Nyongeza ya Mishahara ni Msingi wa Mafao Bora na Kinga Dhidi ya Hali Ngumu ya Maisha”

Watumishi wa Wizara ya Fedha wakiwa tayari kuanza maandamano kuelekea Viwanja vya Jamhuri, jijini Dodoma kwenye Sherehe za Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani, yaliyofanyika kwa ngazi ya Mkoa katika Viwanja hivyo, jijini Dodoma, yakiwa na kaulimbiu ya “Nyongeza ya mishahara ni Msingi wa Mafao Bora na Kinga Dhidi ya Hali Ngumu ya Maisha”

Baadhi ya Watumishi wa Wizara ya Fedha wakiwa wakiwa tayari kushiriki Sherehe za Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani, yaliyofanyika kwa ngazi ya Mkoa katika Viwanja Viwanja vya Jamhuri, jijini Dodoma, yakiwa na kaulimbiu ya “Nyongeza ya mishahara ni Msingi wa Mafao Bora na Kinga Dhidi ya Hali Ngumu ya Maisha”

Baadhi ya Watumishi wa Wizara ya Fedha wakiwa katika maandamano wakati wa  Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani, yaliyofanyika kwa ngazi ya Mkoa katika Viwanja vya Jamhuri,  jijini Dodoma, yakiwa na kaulimbiu ya  “Nyongeza ya mishahara ni Msingi wa Mafao Bora na Kinga Dhidi ya Hali Ngumu ya Maisha”

Baadhi ya Watumishi wa Wizara ya Fedha wakifurahia jambo wakati wa  Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani, yaliyofanyika kwa ngazi ya Mkoa katika Viwanja vya Jamhuri,  jijini Dodoma, yakiwa na kaulimbiu ya  “Nyongeza ya mishahara ni Msingi wa Mafao Bora na Kinga Dhidi ya Hali Ngumu ya Maisha”

(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Fedha- Dodoma)

 Katika kuadhimisha Siku ya Wafanyakazi Duniani maarufu kama Mei Mosi, Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), leo tarehe 01 Mei, 2024 imetembelea Kituo cha Watoto wenye uhitaji cha CHAKUWAMA kilichopo Sinza jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kutoa msaada wa vifaa mbalimbali.

Akikabidhi msaada huo  kwaniaba ya Afisa Mtendaji Mkuu wa BRELA, Afisa Habari Mkuu Bi. Christina Njovu alieleza kuwa Wakala imetoa msaada huo ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa sera  ya kurudisha kwa jamii ambapo wakala imekuwa ikiitekeleza mara kwa mara.

Baadhi ya vifaa vilivyokabidhiwa ni pamoja na vyakula vikiwemo unga, sukari,vifaa vya usafi na vifaa vya shule 

Naye Mkuu wa Kituo cha CHAKUWAMA  Bw. Hassan Hamis ameishukuru BRELA kwa kufika kituoni hapo kuwatembelea na kwa msaada uliotolewa ambao umewapa faraja kubwa ikizingatiwa kwamba hivi karibuni wamepatwa na janga la moto kwa kuunguliwa na bweni la kulala Watoto.

Aidha Bw. Hamis ameeleza kuwa, Kwa sasa kituo kina watoto 72 wa jinsia zote wenye umri tofauti kuanzia chini ya mwaka mmoja hadi miaka 19 na wengi wao wanasoma shule ya msingi na sekondari na kwamba changamoto zao ni nyingi hivyo ujio wa BRELA na vifaa ilivyotoa vitapunguza ukali wa  baadhi changamoto zinazowakabili.

Akielezea historia ya kituo hicho Bw. Hamis.amesema kuwa, Kituo kilianza mwaka 1998 kikiwa na Watoto 5 chini ya mwanzilishi Bi. Saida Hassan kikitumia nyumba ya kupanga eneo la Mikocheni ,  Kituo kimesajiliwa na kinafanya kazi kwa karibu na Wizara ya maendeleo ya jamii, jinsia Watoto na makundi maalum.

Na kuongeza kuwa kituo kina watoto aliowatenga katika  makundi sita wakiwemo,  yatima waliopoteza wazazi wote wawili,  Watoto waliopoteza mzazi mmoja, wapo waliotolewa kwenye mazingira hatarishi na wale waliofanyiwa ukatili na walio okolewa kutoka biashara haramu ya usafirishaji wa binadamu pamoja na walemavu. 

Katika Watoto 72 watoto 60 wanasoma katika ngazi tofauti kuanzia chekechea, msingi, sekondari, veta na vyuo  katika  shule za serikali na shule binafsi za kulipia. 

Aidha Bw.Hamis ameeleza kuwa moja ya changamoto wanazokabiliana nazo ni pamoja na Watoto 12 wamesimamishwa kuendelea na masomo kutona na kuathilika kiakili kulikotokana na ukatili waliofanyiwa na wengine kupata magonjwa na hivyo wanaendelea na matibabu. 

Mbali ya kutembelea kituo cha Watoto wahitaji, BRELA pia imeshiriki katika maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani iliyobebwa na kaulimbiu Nyongeza ya mishahara ni msingi wa mafao bora na kinga dhidi ya hali ngumu ya maisha.




Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akihutubia Viongozi na Wafanyakazi kutoka Wizara, Taasisi za Serikali na Binafsi wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani ambayo Kitaifa yamefanyika katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid Mkoani Arusha tarehe 01 Mei 2024.

Viongozi mbalimbali wa Serikali na Sekta Binafsi wakiwa kwenye Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani ambayo Kitaifa imefanyika katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid Mkoani Arusha tarehe 01 Mei 2024.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akizindua Gazeti la Mfanyakazi Tanzania wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani ambayo Kitaifa yamefanyika katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid Mkoani Arusha tarehe 01 Mei 2024. Kushoto ni Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa na kulia ni Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA) Tumaini Nyamhokya.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akionesha Gazeti la Mfanyakazi Tanzania mara baada ya kulizindua wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani ambayo Kitaifa yamefanyika katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid Mkoani Arusha tarehe 01 Mei 2024.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akitoa zawadi ya ujumla kwa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi ambao wameongoza katika michezo mbalimbali katika kuadhimisha ya Siku ya Wafanyakazi Duniani ambayo Kitaifa imefanyika katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid Mkoani Arusha tarehe 01 Mei 2024.

Na Mwandishi Wetu, Arusha

MKUU wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda ametoa wito kwa Kampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) kuhakikisha fedha zinazotolewa na kampuni hiyo kutekeleza miradi mbalimbali ya kijamii (CSR) zinagusa na kubadilisha maisha ya wananchi wa mkoa wa Geita na Tanzania kwa ujumla.

Mbali na kuipongeza GGML kwa kuja na tenolojia mbalimbali za uokoaji katika maonesho ya Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa kazi (OSHA) yanayoendelea kwenye viwanja vya General jijini Arusha, pia alieleza kuridhishwa na elimu inayotolewa kwa wananchi kuhusu masuala ya afya na usalama mahali pa kazi.

Makonda ambaye alitembelea banda la GGML katika maonesho hayo jana alisema mara nyingi maisha ya watu wa Geita hayafanani na utajiri uliopo katika mkoa huo.

“Mimi sioni aibu kuitwa tajiri,kwa sababu hilo ni jambo la Kujivunia hivyo siwezi kujivunia umaskini ndio maana nataka ninyi Watanzania mliopo kwenye mgodi huu kuendelea kuwa chanzo cha mabadiliko ya watanzania wenzenu wanaozunguka mgodi huu,” alisema.

Aidha, Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi alimpatia maelezo Makonda kwamba mpango wa CSR wa mwaka huu ni mwendelezo wa mipango ya awali unaolenga kujumuisha maendeleo yaliyofikiwa na GGML hadi sasa katika maeneo ya mazingira, miundombinu, afya, elimu na biashara ndogondogo na za kati (SMEs) katika jamii ya mwenyeji wa Geita.

Dk. Kiva alitoa mfano kuwa mwaka jana GGML imesaini Mkataba wa Makubaliano (MoU) na wenyeji wake Halmashauri ya Mji Geita, Wilaya ya Geita pamoja na Halmashauri za jirani za wilaya za Chato, Bukombe na Mbogwe kutekeleza Mpango wa Uwajibikaji wake kwa Jamii (CSR) kwa mwaka 2022/2023 wenye thamani ya Sh bilioni 19.

“Jumla ya Sh bilioni 9.8 zilitengwa kwa ajili ya Halmashauri ya Mji wa Geita ambapo kwa Halmashauri ya Wilaya ya Geita, bajeti ya Sh bilioni 8.6 ilitengwa.

“Uwepo wa GGML katika mkoa wa Geita umeonyesha matokeo chanya katika sekta ya elimu baada ya kampuni hiyo kujenga miundombinu zaidi ya 1800 ya shule za msingi na sekondari katika wilaya ya Geita yenye halmashauri mbili za Geita mji na ile ya wilaya ya Geita,” alisema.

Alisema miundombinu hiyo imetokana na utekelezaji wa mabadiliko ya sheria ya madini ya mwaka 2017 ambapo GGML imekuwa ikiandaa mpango wa huduma kwa jamii kwa kushirikiana na halmashauri husika huku kila mwaka hutenga kiasi cha Sh 9.2 bilioni kwa ajili ya miradi ya maendeleo.

Mbali na miradi ya elimu, Dk. Kiva alisema GGML kupitia fedha za CSR walitenga fedha kwa ajili ya miradi ya mazingira ambapo kiasi cha Sh700 milioni zinatumika.

“Ipo pia miradi ya kimkakati ukiwemo ule wa ufugaji wa samaki, miradi kwa kinamama na vijana pamoja na wasiojiweza ambapo zaidi ya Sh1.5 bilioni zinatumika.

Alisema miradi hiyo inaongeza thamani katika sekta mbalimba za kiuchumi na kuwapatia wananchi maendeleo.

 

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (kushoto) na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira wa GGML, Dk Kiva Mvungi (kulia) wakifurahia jambo katika banda la GGML wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha. Katika Maonyesho ya OSHA 2023, Geita Gold Mining ilitambuliwa kama kampuni iliyofanya vizuri zaidi katika masuala ya afya na usalama kazini, na pia ilitunukiwa tuzo ya muonyeshaji bora kwa ujumla.

Watumishi Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu leo tarehe 1 Mei, 2024 wameshiriki maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi (Mei Mosi) yaliyofanyika kimkoa katika Uwanja wa Jamhuri, jijini Dodoma.

Maadhimisho hayo hufanyika kila mwaka ifikapo tarehe 1 Mei ambapo kwa mwaka huu kitaifa yamefanyika Jijini Arusha na Mgeni Rasmi alikuwa Makamu ya Rais, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango.






Top News