Home
Unlabelled
kikao
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Most read Swahili blog on earth
Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.
hapa sio river kweli maana ndo almaaruf place kwa vikao
ReplyDeleteMtaje. ili kama twamfahamu tuchangie chochote hapo...!
ReplyDeleteMichuzi habari. Unaweza kuweka ujumbe huu wa MICHANGOOOOOOOO, kutokana na hiyo picha yako ya kikao cha maandalizi ya harusi ya huyo mdau mwenzenu.
ReplyDeleteMICHANGO ah Mungu wangu. Nchi gani hii kila ukiamka, kila ukiwa njiani, ofisini au ukilala ni kusakamwa na michango tu?
Michangooo, michangooo na michangoo! Twatolewa genii mpaka
tumepata pancha.
Hapana naapa! Kwa sasa mmezidi. Amka asubuhi utasikia hodi,
ukifungua kuna mtoto na kikadi kilichoburuzwa kwenye kompyuta
kikiomba mchango wa "kitchen party." Yarabi!
Unamwambia utawasiliana na baba yake anaondoka. Upo kwenye daladala unawahi Pugu Road kazini, unaombwa samahani na mtu akidai alikuwa na barua yako na anakupatia bila hiana.
Mtumeee! Unafungua unakuta ni kakadi kengine ka mchango.
Safari hii ni ka "chicken party na kameonyesha kiwango kabisaa.
Kwa fasheni ya sasa ni 7,000/-. Huyu ni wa aibu, hivyo unampa
tano ukidai mbili utamtuma mtoto.
Unatoka kazini hujala chochote kwa vile 5,OOO/= ulitoa kwenye
"chicken party" ambayo hata maana ya neno lenyewe hujui. Unakuta
kengine nyumbani. Hako ni ka mchango wa "send off'. Jamani
wanitakani?
Unaoga, ghafla aja mtu na kadi tena safari hii ni mchango wa
harusi ya shemejiyo. Unajikamuakamua ili usiadhirike ukweni, unampatia kiasi kilichokuwa ada ya mtoto wa dada yako aliyemtelekeza kwa wazazi wako shuleni.
Hayo bado kuhudhuria vikao vya shemejio vya harusi nako kuna
kamchango ka kila mkutanapo kanaitwa uchache au chakaza.
Shemeji mtu tena si ni lazima wakukamue kamasi mwanangu?
Haiishii hapo, unakuja ujumbe kuwa dada yake dada wa mama
yako mzazi kafia Muhimbii yuko mochwari. Hapo achilia mbali
bakuli la mchango utakalokuta, patakuwepo pia kitabu cha
kujiorodhesha na kiasi mtakachotoa.
Michango haitoshi, sasa yabidi wale wa karibu yake mjazie ili
iwezekane kukodisha "Fuso" ya kusafirishia maiti. Na huko nyumbanl ni lazima mkamuliwe tena hela ya kununulia mboga.
Unasema walau sasa napumua, Inatoka barua kwa wajomba zako kuwa
ile arobaini ya babu ni mwezi ujao, Hapo yataka mchango wa
kununulia ng'ombe na mchele kwa ulaji wa siku hiyo.
Kwani utakimbia jamii yenu kwa vile imekuwa ya michango? Kazini
wameanza kukukata mshahara kwa madeni uliyo nayo SACCOS. Mtoto
wa jirani ambaye umemdhamini ubatizo naye aja akidai mchango wa
kunuunulia gauni la "birthday".
Ebo! Sasa mwanangu? Utasahau mdogo wenu wa mwisho alipigwa
retrenchi na sasa ana mtoto mchanga wa kubatiza. Utakwepa vipi
usimchangie kitu kidogo atakapowahi kwako majogoo?
Afadhali usingezaliwa Kipatimu mwanangu. Mwezi huu ni wa kuwacheza
watoto. Utawaambia nini huko kwenu wakuelewe kama hukutuma mchango
wa hilo tamasha?
Bado wana wewe kaka! Mtoto wa kaka yako anapata komunio utamkwepaje
mbele ya jamii iliyokuzunguka? Afadhali tajiri yako asingekuwa na
mtoto Chuo Kikuu anayegradueti na keshakuletea kadi ya mchango.
Utachanga sana graduesheni ya sekondari, chekechea hata na darasa
la saba achilia mbali VETA. Mtajiju wenyewe, nani aliyewatuma
kuzaliwa Bongo, Afadhali wanajeshi hawana sherehe hata wapatapo
umeja.
Utadhani sasa utapumua uendapo nyumba za ibada, Yallaaah! Utakutana na michango ya ofisi ya paroko, mchango wa jengo na pikipiki ya shemasi. Mpo hapo?
Kijijini ndo usiseme tena. Kuna barabara, shule, maji, zahanati, ugeni wa DC, vyote vyadai mchango na mara nyingi hakuna risiti. Si ni jamaa zako una wasiwasi gani?
Umesahau mfereji wa kijiji, trekta la mshikamano vyote vyataka
michango achilia mbali mchango wa damu Muhimbili! Afadhali huu wa damu kwa vile hauhusu fedha.
Unafikia mahali unasema utapanchi hiyo michango. Ukiwaza hayo,
mara anapita Katibu kata mwenyewe. Huyu anadai mchango wa mapokezi
ya Waziri Mkuu au ya Mwenge utasemaje?
Hakuna huruma na mtu wala hakuna wa kutaka kujua kipato chako kabla
hajakupa kadi ya mchango. Shuleni watatuma barua kuhusu mchango wa
kumwaga mwalimu mkuu. Bado michango ya tuisheni, uji wa saa nne, michezo ya UMISHUMTA, safari ya Serengeti na T-shirt za shule. Mmesahau redio ya shule ikikosa betri wazazi shurti, wachangishwe? Mwashangaa nini hospitalini hamchangii?
Michango hii! Sasa mtatukamua damu. Ipo ya kwaya, Saidia Simba/Yanga Ishinde,usafi wa makaburi, basi la kijiji. Bado sijasema makato/michango ya SACCOS na upatu kazini kwenu.
Kzi kweli kweliiiiii
Zumba's
Zumba umelonga ukweli.
ReplyDeleteIla mimi kinachoniua sana ni ile ya wananchi ukiwa an mgonjwa hakuna yeyote atakayethubutu kukupa mchango hata kama ukiomba ila ikitoke mgonjwa wako akafariki hao hao watakuja na michango ili kufanikisha mazishi ya kifahari
Sir Issa UJUMBE TUMEUPATA mimi nataka kutoa mchango...NIMTAFUTE NANI HAPO ?? KAMA NINAONA SAWA SAWA, CHUPA ZAMAJI HAPO MEZANI NI MBILI TU KAKA...PICHA INAPENDEZA.
ReplyDelete