TAARIFA KWA WANAJUMUIA YA WATANZANIA WAISHIO DELHI
Ubalozi wa Tanzania Nchini India- New Delhi, unawakaribisha Watanzania wote kujumuika katika kusaini kitabu cha maombolezo ya Waziri Mkuu na Makamu wa Rais wa Awamu ya kwanza, Mpendwa wetu RASHID MFAUME KAWAWA maarufu SIMBA WA VITA aliyetutoka hivi karibuni.
Kitabu cha Maombolezo kitakuwepo Ubalozini eneo la Chanakyapuri EP 15 kwa ajili ya Watazania wote kuanzia saa Tano Asubuhi MPAKA Jioni kuanzia Kesho Alhamisi JANUARY 7TH Hadi Ijumaa JANUARY 8TH.
Wote Mnakaribishwa kutoa heshima hiyo Muhimu.
Mungu Ailaze Roho ya Marehemu RASHID MFAUME KAWAWA .AMEN.
Mwenyekiti wa Tasa - New Delhi
Jennifer Sumi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...