MSIMU MPYA LIGI KUU YA VODACOM
Msimu mpya wa Ligi Kuu ya Vodacom 2011/2012 unaanza kesho (Agosti 20 mwaka huu) ambapo timu 10 kati ya 14 zinazoshiriki katika ligi hiyo zitakuwa viwanjani. Mechi za kesho ni Coastal Union v Mtibwa Sugar (Mkwakwani, Tanga), Kagera Sugar v Ruvu Shooting (Kaitaba, Bukoba), Toto Africans v Villa Squad (Kirumba, Mwanza) na Polisi Dodoma v African Lyon (Jamhuri, Dodoma).
Mechi nyingine ni Azam v Moro United itakayochezwa Chamazi, Dar es Salaam wakati mechi za Jumapili (Agosti 21 mwaka huu) ni Oljoro JKT v Simba (Sheikh Kaluta Amri Abeid, Arusha), na Yanga watakaokuwa wenyeji wa JKT Ruvu.
WAAMUZI WA KATI
Waamuzi wa kati (centre referees) 16 wameteuliwa kuchezesha Ligi Kuu. Waamuzi hao ni Ronald Swai (Arusha), Isihaka Shirikisho (Tanga), Peter Mujaya (Mwanza), Amon Paul (Mara), Mathew Akrama (Mwanza), Ibrahim Kidiwa (Tanga), Dominic Nyamisana (Dodoma), David Paul (Mtwara), Hashim Abdallah (Dar), Martin Saanya (Morogoro), Orden Mbaga (Dar), Kennedy Mapunda (Dar), Israel Mujuni (Dar), Alex Mahagi (Mwanza), Abdallah Kambuzi (Shinyanga) na Thomas Mkombozi (Kilimanjaro).
Pia wameteuliwa waamuzi wa akiba (reserve referees) sita ambao watatumika wakati wowote watakapohitajika. Waamuzi wasaidizi (assistant referees) walioteuliwa kuchezesha ligi ni 34. Kwa upande wa waamuzi wasaidizi wa akiba walioteuliwa ni kumi. Hivyo jumla ya waamuzi watakaotumika kwenye ligi hiyo ni 50.


Kwa habari hizi na nyingine kibao za TFF leo
BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...