KARIBUNI KATIKA BLOG YA WANAFUNZI WOTE 
POPOTE TANZANIA (MATUKIO NA WANAVYUO)

Kwanza tunapenda kuwasalimu sana Ndugu walimu na wanafunzi na wadau wote mliopo popote nchini Tanzania na Duniani kwa ujumla.

 Kwa heshima na Taadhima tunapenda kuwatambukisha kwenu Blog mpya kabisa inayo kwenda kwa jina la MATUKIO NA WANAVYUO ambapo lengo kubwa ni kuwakutanisha wanavyuo wote Nchi nzima na kubadilishana mawazo pia kujua nini kinaendelea kila wakati kupitia mtandao huu.

Hatuna mengi sana ya kuandika hapa kwa maana mtandao wenu unajieleza vizuri kabisa. Pia mtandao huu ni wanavyuo wote waliopo vyuoni sasa na wale walio maliza pia ni wa watanzania wote kwa ujumla kwa maana kuna mambo yanayo wahusu na muhimu. 

Tunawaomba mpitie kila kona ya mtandao huu na kutoa maoni kama yapo nini kiongezwe ama kuboreshwa zaidi, Tunawakumbusha tena mtandao huu ni wako. sisi tunaongoza tuu kwa mawasiliano zaidi tutumie Barua pepe kupitia 


tunatanguliza  shukrani zetu pia atakae pata taarifa hii ampe na mwenzakeAsanteni sana.Matukio na wanavyuo Crew KUTEMBELEA MTANDAO HUU BOFYA HAPA http://www.tzwanavyuo.blogspot.com/

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 5 mpaka sasa

  1. Lengo lingine liwe pia kuweka kumbukumbu ya michango mbalimbali ya kimawazo au mali ambayo hutolewa na wanavyuo (waalimu, wanafunzi na waliowahi kupita katika vyuo)kwa maendeleo ya taifa hili.

    ReplyDelete
  2. Lakini mbona sijaona promotion vyuo vingine kama vile Sokoine University, Ardhi University na MUHAS (Muhimbili)?

    ReplyDelete
  3. wadau tunawaomba kama mna Taswira ya hivyo vyuo mtutumie pia tutaweka moja kwa moja pia tunapokea matukio kutoka vyuo vyote na taarifa mbali mbali.. Huu ni mtandao wenu tumeni kupitia twanavyuo@live.com hatuna upendeleo wowote. wala ubaguzi wa chuo fulani

    ReplyDelete
  4. Mh! wathomi wetu, hawachelewi kujiita kembriji ya tanzania hawa.

    ReplyDelete
  5. Tunaomba wanavyuo mtuambie maana ya neno "libeneke" ni nini? Sijui kama ni neno la kiswahili sanifu au ni la mtaani. Kumbukeni hii blog ni ya wasomi kwa hiyo hatutarajii muungane na watu wengine kuharibu kiswahili. Tunatarajia blog hii iwe tofauti na blog zingine hasa ukizingatia kwamba ninyi ni wasomi na humu mtatoa ilmu.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...