wachezaji wa timu ya bunge mara baada ya kumaliza mazoezi kwenye uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma wakipata maelezo kutoka kwa nahodha wa timu hiyo Idd Azan, mwenye miwani ni kocha msaidizi Abdul Mteketa.
Kiungo mchezeshaji wa timu ya Bunge, Stephen Ngonyani 'Profesa Majimarefu' akijaribu kuzuia mpira kwenye mazoezi ya timu hiyo yanayofanyika kwenye uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma, Timu hiyo ya bunge inajiandaa na michuano ya mabunge ya afrika mashariki michuano itakayoanza Novemba 20 nchini Burundi.
Mchezaji wa kutumaini wa timu ya bunge sports, Mahamoud Mgimwa akichuliwa na daktari wa timu hiyo dkt cesilia sanya baada ya kupata majeruhi kufuatia mazoezi ya timu hiyo inayojiandaa na mashindano ya mabunge ya afrika mashariki yatakayofanyika nchini burundi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 10 mpaka sasa

  1. namkumbuka huyo mudi alikuwa beki 3 wa akiba pale JKT mafinga OPERATION NIDHAMU 1986-87 almaarufu kama mudi vitumbua big up mbunge

    ReplyDelete
  2. Ivi hakuna daktari wa kiume kumchua huyo mbunge; mbona mnaleta mambo zenu za ajabu - uyo kazidisha maumivu baada ya kuona daktari wa kike angekuwa wa kiume angepona bila kuchuliwa

    ReplyDelete
  3. Kikosi cha Bunge la Tanzania kinaundwa na Wabunge pamoja na Watumishi wa Ofisi ya Bunge ni kikosi imara na kwa taarifa tu Bunge la Tanzania ndio mabingwa watetezi wa Michuano ya Mabunge ya Afrika Mashariki ambayo kwa mara ya mwisho, ilifanyika Arusha 2009. Kila la heri kwa timu yetu, ituwakilishe vyema na kutetea ubingwa.
    Mdau

    ReplyDelete
  4. hakuna timu hapo uzushi tu wengine hapo ndo nitoke vipi mkiwa bungenihamna kitu hata mpira uzushi mtupu

    ReplyDelete
  5. sasa mbona mdada anatoa huduma ya 1 hata bila kuvaa gloves?

    ReplyDelete
  6. DA, MASSAGE HIYO......

    ReplyDelete
  7. na hiyo timu profesa mwenyewe maji marefu yumo ndani ikifungwa ndio basi tena!

    ReplyDelete
  8. Ankali mbona beki sugu hatujamuona na timu meneja mzee cheyo hayupo?

    mbona kamati ya ufundi mzee mrema hayupo?

    hapo timu haijakamilika bado

    ReplyDelete
  9. Jamani wingi (plural) ya bunge si mabunge=wabunge

    ReplyDelete
  10. Sawa "walanchi" sasa hivi mnacheza ili kupunguza mafuta ya mlivyokula, sisi "wananchi" tunatoka jasho la damu kwani mafuta hatuna.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...