Dj Machachari aliekuwa akifanya kazi kwenye kampuni ya InterGrated Communications LTD,Amos Dotto amefariki Dunia leo asubuhi wakati akiwa safarini mkoani Tabora kuelekea nyumbani kwao Ushi Rombo mkoani Shinyanga.

Marehemu Amosi amefikwa na mauti hayo kutokana na Maradhi yaliyokuwa yakimsumbua kwa muda mrefu,Kwa sasa mipango ya mazishi inapangwa kwa ushirikiano wa ndugu,jamaa,marafiki na wafanyakazi wenzake wa kampuni hiyo ya InterGrated.

Amosi katika uhai wake alikuwa Dj maarufu wa vipindi mbalimbali katika vituo vya runinga.Aidha alikuwa Dj maarufu wa Kampuni hiyo ya Integrated hasa kwenye promosheni mbalimbali zinazoendeshwa na kampuni hiyo.

Kupitia Globu ya Jamii tunaomba kuwafahamisha wanajamii na hasa wanataaluma ya habari na Djs wote kuhusu msiba huu mkubwa

Bwana Ametoa na Bwana Ametwaa,Jina la Bwana Lihimidiwe.

Amein.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Ni mashaka sana kumpoteza kijana katika umri huu,Mungu uwape nguvu wazazi na ndugu zake katika kipindi hiki kigumu...pumzika kwa amani Dj Amos!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...