Hospitali ya Taifa Muhimbili imeandaa mkutano na wadau utakaofanyika Oktoba 9, 2012 saa 04:00 asubuhi katika ukumbi wa Karimjee.

Lengo la mkutano huu ni kutaka kupata maoni ya moja kwa moja  kutoka kwa wananchi tunaowahudumia kuhusu kuridhika au kutoridhika kwao na huduma tunayotoa. Wananchi wataeleza ni maeneo gani hawaridhiki nayo na pia watapata fursa ya kushauri nini kifanyike ili  kuboresha huduma za tiba, uchunguzi, upasuaji n.k

Hospitali inatoa huduma kwa wagonjwa wa nje wasiopungua 1,000 hadi 1,200 kwa siku na wagonjwa waliolazwa kwa wakati wote wodini ni kati ya 1,000 hadi 1,200 kwa siku.

Hospitali imeonelea ni wakati muafaka wananchi kutumia fursa hii kushiriki katika mkutano huu kutoa maoni yao moja kwa moja.

Mkutano huu utahudhuriwa na Menejimenti ya Hospitali ikiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji ambayo ndiyo yenye dhamana na kusimamia utendaji wa kila siku wa Hospitali.

Wakuu wa Idara zote ambazo huduma zinatolewa katika maeneo yao watakuwepo katika Mkutano huo ili kusikia moja kwa moja kutoka kwa wananchi juu ya utendaji wa idara zao kwa wananchi wanaowahudumia.

Tunaomba kuchukua fursa hii, kwa dhati kabisa kuwaalika wananchi kufika na kushiriki kikamilifu katika mkutano huu ili kutoa maoni yao. Tunaamini kuwa maoni yao ni ya muhimu sana na ndiyo maana tumetoa fursa hii ili tupate mrejesho wa moja kwa moja kutoka kwa wadau tunaowahudumia.

Kama kuna swali lolote ambalo mwananchi angependa kuuliza kabla ya mkutano huo anaweza kutuma kupitia barua pepe info@mnh.or.tz nasi tutalifanyia kazi na kutoa majibu siku hiyo hiyo ya mkutano. Aidha unaweza kutuma maoni yako kwa njia ya posta kwa Mkurugenzi Mtendaji, Hospitali ya Taifa Muhimbil, S. L. P. 65000 Dar Es Salaam. Tutaipokea barua yako na tutaijibu.

Ndugu wananchi, tunarudia tena kuwaomba kushiriki kikamilifu katika mkutano huu ili kutoa maoni yenu juu ya huduma mablimbali zitolewazo na hospitali ya taifa. Karibuni sana..

Imetolewa na Ofisi ya Uhusiano
Hospitali ya Taifa Muhimbili
Oktoba 4, 2012

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Naomba mpokee maoni yangu kwa mtandao.

    Hii ni nzuri, ila nasikitika nitaikosa kwa kuwa mbali na mkoa.

    Mimi ni mdau mkubwa hospitali hii Muhimbili. Nashukuru kwa kuanzisha huduma zenu za PRIVATE ambazo kama sijakosea mnaziita IPPM. Najua mlianzisha hii kwa lengo zuri. Sasa huduma hii ya private (IPPM) naomba muiboreshe hata ikiwezekana iendane na fedha zilipwazo.

    ReplyDelete
  2. mimi mni mdau original wa hospitali ya muhimbili,ndugu zangu kama 10 hivi wemefia hapo.mkutano huu uko kwenye taratibu za kisheria za kazi au ni yale yaleeh, mtu mmoja tu clever boy anawaburuza wengine !
    kama ni heri hongereni saana !

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...