Naibu Katibu Mkuu mstaafu wa Umoja wa Mataifa, Dk. Asha Rose Migiro (katikati) mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi milioni tano kutoka kwa Mkuu wa Kitengo cha Masoko wa Benki ya KCB Tanzania, Christiane Manyeye (kulia) na mwakilishi wa ubalozi wa Kenya, Boniface Makao wakati wa harambee ya kuchangisha fedha kwa ajili ya ujenzi wa mabweni ya wanafunzi wa kike iliyofanyika jijini Dar es Salaam juzi. Wa pili kushoto ni Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa.
Miss Tanzania 2005, Nancy Sumari akikabidhi mchango wa dola za kimarekani 1,000 kwa  Aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Dk. Asha Rose Migiromgeni ambaye alikuwa mgeni rasmi katika harambee ya kuchangisha fedha kwa ajili ya  ujenzi wa mabweni ya wanafunzi wa kike iliyofanyika jijini Dar es Salaam
Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, mstaafu Dk. Asha Rose Migiro (kushoto) akimkabidhi cheti cha shukrani, Mkuu wa Kitengo cha mahusiano wa Shirika la Nyumba (NHC), Susan Omari baada ya shiriki hilo kuchangia mabati 1,000 yenye thamani ya shilingi milioni 20 kwa ajili ya ujenzi wa mabweni ya wanafunzi wa kike iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
Naibu Katibu Mkuu mstaafu wa Umoja wa Mataifa, Dk. Asha Rose Migiro akipokea mchango wa shilingi milioni tatu kutoka kwa  Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa ukiwa ni mchangop wake kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa mabweni ya wanafunzi wa kike wakati wa harambee ya kuchangia ujenzi wa mabweni ya wasichana iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
Meneja Mawasiliano wa TCRA, Inocent Mungi akikabidhi mchango wa shilingi milioni tano kwa Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa mstaafu, Dk. Asha Rose Migiro wakati wa harambee ya kuchangisha fedha kwa ajili ya ujenzi wa mabweni ya wanafunzi wa kike iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
Mmiliki wa Blog ya 820,  Shamim Mwasha, akitoa mchango wa shilingi laki 6.5 alizokusanya kutoka kwa wasomaji wa mtandao wake.

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. I LOVE YOU SHAMIM MWASHA, AND I LOVE YOU ALL....MMEFANYA VIZURI KUCHANGIA ISSUE YA MAANA SANA HII.SHAMIM MTOTO WA WATU USIYEJUA MARINGO NI NINI, MUNGU AZIDI KUKUBARIKI NA 8020 IZIDI KWENDA MBELE.
    ALL THE BEST

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...