Changchun, Jilin,China

Elimu Maalum kuhusu Uzalendo inabidi itolewe ili kuwafanya watanzania waendelee kuheshimu Uhuru na dhana nzima, hayo yalisemwa na wachangiaji kwenye mjadala mfupi ulioandaliwa ili kuadhimisha miaka 51 ya Uhuru wa Tanzania hapa.

Mjadala huo mfupi, uliofanyika katika Mgahawa wa Chun Yuan Kao Rou Wang jana (Jumapili), ulikuwa umeandaliwa na watanzania wanaoishi hapa, ambao wengi ni wanafunzi kwenye Vyuo Vikuu mbalimbali vilivyopo kwenye jimbo hili.

Walisema kuwa elimu ya Uraia imeonyesha mapungufu makubwa kwa kuwa haiwafanyi vijana kuwa na uzalendo kwa nchi yao, kama ilivyokuwa mwanzo. Walipendekeza kuwa watengenezaji wa mitaala waangalie utengenezaji wa elimu hiyo katika changamoto za uchumi wa soko huria, ambalo linapingana kwa kiasi kikubwa na dhana ya uzalendo.

Walionya kuwa hata mmomonyoko wa maadili na ubinafsi unaolisumbua taifa kwa sasa ni matokeo ya kukosekana kwa elimu hiyo ya Uzalendo.

Wachangiaji Wakuu walikuwa Yazidu Saidi, Hamza Ibrahim, Captain Mwita Vedasto Wambura, Tessua Ally na Albert Memba. Mjadala huo uliratibiwa na Innocent Mugisha.
Watanzania wanaosoma kwenye vyuo vikuu mbalimbali hapa Changchun, Jilin, China wakiwa kwenye picha ya pamoja baada ya mjadala mfupi wa maadhimisho ya 51 ya Uhuru wa Tanzania uliofanyika kwenye Mgahawa wa Chun Yuan Kao Rou Wang Jumapili.
Mchangiaji Yazidu Saidi akizungumza kwenye mjadala mfupi wa Maadhimisho ya Miaka 51 ya Uhuru wa Tanzania uliofanyika kwenye Mgahawa wa Chun Yuan Kao Rou Wang Jumapili.
Mwita Vedasto Wambura akichangia kwenye mjadala wa maadhimisho ya 51 ya Uhuru wa Tanzania uliofanyika kwenye Mgahawa wa Chun Yuan Kao Rou Wang Jumapili.
Mchangiaji Hamza Ibrahim akichangia kwenye mjadala mfupi wa maadhimisho ya 51 ya Uhuru wa Tanzania uliofanyika kwenye Mgahawa wa Chun Yuan Kao Rou Wang Jumapili.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 7 mpaka sasa

  1. Wanajamii, tusikidanganye kizazi kipya au kinachofuatia. Tanzania haijawahi kutawaliwa na wageni, hivyo haijapata uhuru 1961. Iliyopata uhuru 1961 ni Tanganyika au kwa jina jengine la sasa ni Tanzania Bara. Tanzania ni Jamhuri ya muungano wa nchi za Tanganyika iliyopata uhuru wake 1961 na Zanzibar iliyopindua 1964. Tanzania iliunda 1964. Hivyo si sahihi kuandika Tanzania inasheherekea uhuru wa miaka 51.

    ReplyDelete
  2. Mbona Wanaume watupu? Wanawake wapo wapi?

    ReplyDelete
  3. geneder haikizingatiwa ktk mjadala

    ReplyDelete
  4. Uzalendo utachangiwa na mchakamchaka, sanaa, utamaduni, mafunzo ya historia ya kweli ktk shule zote za msingi na sekondari binafsi na za serikali.

    ReplyDelete
  5. Uhuru maana yake nini? au ni kutoka chini ya utawala wa kizungu na kuwa chini ya utawala wa wachache wa waafrika wenzetu?

    Wanazidi kuwa matajiri wao na watoto wao kila kukicha wakati mamilioni tunazidi kuwa 'makapuku'

    Tafakari! Tuchukue Hatua!

    ReplyDelete
  6. HAWA WAKO WAPI?DODOMA AU KCMC?

    ReplyDelete
  7. Wako kishumundu kwani huoni migomba na kahawa kwenye background?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...