Msajili wa Mahakama ya Kimataifa ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda (ICTR), Bongani Majola (katikati) akizungumza na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi (kushoto) kuhusiana na mafanikio na changamoto mbalimbali ya Mahakama hiyo ambayo Makao Makuu yake yapo jijini Arusha. Kulia ni Msemaji wa Mahakama hiyo, Roland Amoussouga.
Msemaji wa Mahakama ya Kimataifa ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda (ICTR), Roland Amoussouga akimfafanulia masuala mbalimbali Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi (kushoto) wakati viongozi hao walipomtembelea waziri huyo ofisini kwake, jijini Dar es Salaam leo. Wa pili kutoka kushoto ni Msajili wa Mahakama hiyo, Bongani Majola. Kulia ni Mwanasheria wa mahakama hiyo, Jerry Mburi.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi akizungumza ofisini kwake na Msajili wa Mahakama ya Kimataifa ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda (ICTR), Bongani Majola (katikati). Ziara hiyo, ambayo pia ilikuwa na lengo la msajili huyo kujitambulisha na kumsalimia Waziri Nchimbi, na kumuelezea shughuli mbalimbali zifanywazo na mahakama hiyo pamoja na kumuelezea changamoto mbalimbali zinazoikabili mahakama hiyo. Hata hivyo, Waziri Nchimbi aliahidi kushirikiana na mahakama wakati wowote itakapohitaji msaada kutoka ofisini kwake.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Ugeni huu wa ICTR umewadia wakati mzuri sana!

    Pia nadhani uamuzi wa kusitisha shughuli zake Mahakama hii uangaliwe upya maana pia humu humu nchini tuna watu wengi tu ambao wanaendesha Mauaji ya halaiki.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...