Mwakilishi wa Kampuni ya Uchimbaji wa Visima ya ZENTAS kutoka Uturuki nchini Tanzania Dkt, Mohammed Akbar Akitoa taarifa za kukamilika kwa kazi ya uchimbaji wa kisima chenye urefu wa mita 541 eneo la Mkwalia, Mkuranga, Pwani leo.Kisima hicho kinauwezo wa kuzalisha maji lita milioni 1.8 kwa siku.
 Maji kutoka katika kisima hicho yakitiririka kufuatia kufanyika kwa majaribio ya kuyatoa maji kutoka ardhini.
 Mtaalam wa mitambo wa Kampuni ya ZENTAS Sahtn Topal ( katikati) akifafanua teknolojia na vifaa vilivyotumika kuchimba kisima hicho.Picha na Aron Msigwa/ MAELEZO.

Na.Aron Msigwa- MAELEZO
Wananchi wa wilaya ya Mkuranga,mkoa wa Pwani wanatarajia kunufaika na mradi mkubwa wa usambazaji wa maji kufuatia kukamilika kwa zoezi la uchimbaji wa kisima cha maji chenye urefu wa mita 541 ambacho kina uwezo wa kuzalisha lita milioni  1.8  kwa siku.

Akitoa taarifa za kukamilika kwa kazi ya uchimbaji wa kisima hicho  mwakilishi wa kampuni ya kuchimba visima ya ZENTAS  kutoka Uturuki nchini Tanzania Dkt.Mohammed Akbar amesema wao kama wataalam wanaendelea na majaribio ya kuyatoa maji kutoka ardhini  jambo ambalo limeonyesha mafanikio makubwa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...