Viongozi na Wafanyakazi wa Benki ya CRDB Tawi la Lumumba, wakijiandaa kushuka chini kwenye jengo la Lumumba ili kuwapokea watoto kwa sherehe ya Siku ya Mtoto Afrika iliyosherehekewa tawini hapo leo mchana. Wazazi kote nchini, wamehimizwa kuwajengea watoto, tabia ya kuweka akiba, kwa kuwafungulia Akaunti maalum za Watoto, ili kuzitumia fedha hizo katika kugharimia Elimu. 
Wito huo, umetolewa na Mkurugenzi wa CRDB Tawi la Lumumba,  Bibi Pendo Assey wakati wa kuadhimisha siku ya  Mtoto wa Afrika, katika Tawi hilo hapo.
Bibi  Assey amesema, Tanzania ina watu wengi, lakini watu wanaohudumiwa na huduma za kibenki ni watu wachache, kutokana na Watanzania kutokuwa na utamaduni wa kujiwekea akiba, hivo kuwafungulia Watoto akauti, kutawajengea utamaduni wa kujiwekea akiba.
 Viongozi na Wafanyakazi wa Benki ya CRDB Tawi la Lumumba, wakijiandaa kuwapokea watoto kwa sherehe ya Siku ya Mtoto Afrika iliyosherehekewa tawini hapo leo mchana.
  Mkurugenzi wa Utawala na Manunuzi wa Benki ya CRDB, Beatus Segeja,(Kulia) akikata keki wakati wa sherehe ya Siku ya Mtoto wa Africa, CRDB Bank, Tawi la Lumumba.
 Baadhi ya watoto na mabango yenye ujumbe muhimu
Mkurugenzi wa CRDB Tawi la Lumumba,  Bibi Pendo Assey akikata keki wakati wa kuadhimisha siku ya Mtoto wa Afrika, iliyoadhimishwa leo tawini hapo. Kwa picha zaidi BOFYA HAPA





Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 17, 2016

    CRDB naona wamejipanga kweli kweli kuimarisha Benki

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...