Ma DJ’ maarufu Afrika Kusini Siyabonga Sibeko ‘DJ Capital’ na  Lutendo Kungoane ‘Dj Sliqe’  wakizungumza na waanadishi wa habari hawapo pichani, Dar es Salaam jana kuhusiana na ziara yao ya wiki moja nchini katika kujifunza vitu tofauti vya kimuziki.

Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii


Ma DJ’ maarufu Afrika Kusini Siyabonga Sibeko ‘DJ Capital’ na Lutendo Kungoane ‘Dj Sliqe’ wamesema  kwa sasa muziki wa Tanzania upo vizuri na utafika mbali kama wasanii watajituma zaidi na kuweza kuufikisha kimataifa.

Wakizungumza na Waandishi wa Habari jana katika hoteli ya New Africa Jijini  Dar es Salaam, ma DJ hao kutoka  redio na  vituo vya luninga nchini Afrika Kusini walisema kwa sasa Tanzania imepiga hatua kubwa kimuziki katika hatua  

“Kwa sasa huwezi kuzungumzia nchi zinazofanya vizuri kwa kiwango cha juu kimuziki Afrika bila kuitaja Tanzanja,”alisema Dj Capital na kuongeza “Afrika Kusini, Nigeria, Ghana, Tanzania na Kenya hizo ndizo nchi za Afrika zinazofanya vizuri katika muziki wa kisasa,”alisema. 

“Tumekuja hapa kujigunza na kukutana na wasnaii kwa sababu sisi pia ni watayarishaji wa muziki,”alisema Capital. 


Kwa upande wake DJ Sliqe’ alisema kwamba anavutiwa zaidi na wasanii wawili wa Tanzania kwa sasa, ambao ni Diamond Platnumz na Vanessa Mdee na  huku akisisitiza kuwa kuna  wasanii wengi wa Tanzania wanaofanya vizuri kwa sasa, lakini kwa  upande wake anawapenda zaidi hao wawili.

Wawili hao, wote ni Ma DJ wa kituo cha Redio cha Touch Central cha Johannesburg, Afrika Kusini wakati DJ Capital pia anafanya kipindi cha Club 808 cha Televisheni ya ETV nchini humo na wamekuja nchini kwa ziara ya wiki moja kujifunza zaidi kuhusu muziki wa Tanzania, pia ni Ma DJ wa kumbi za disko nchin kwao. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...