Na Chalila Kibuda , Globu ya Jamii 

Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigamboni , Stephen Katemba amesema kiwanda cha Lake Cement kinafuata sheria za utunzaji wa mazingira kwa wananchi wa Kimbiji. 

Katemba amesema hayo wakati alipokwenda kusherekea siku ya wafanyakazi na kushiriki shughuli mbalimbali za kijamii zinazofanywa na Lake Cement, amesema kuwa kiwanda kwa kufuata sheria ya mazingira na sheria za wafanyakazi kamwe migogoro haiwezi kutokea. 

Amesema kuwa wafanyakazi lazima wafanye kazi kwa kujituma ili kiwanda kiweze kujiendesha katika kuweza kufikia malengo ya kutimiza kwa wafanyakazi wake. 
Katemba amesema wakati kitendo cha Kiwanda kudhamini mashindano mbalimbali katika eneo la kimbiji ni kuonyesha kiwanda kinajua wajibu wake. 

Makamu wa Rais wa Lake Cement , Afroz Ansary amesema wanawajibu wa kuwa karibu na jamii ya Kimbiji katika shughuli za kijamii . Mafanikio ya kiwanda yanatokana na jamii inayozunguka kushirikiana katika masuala mbalimbali ya kijamii. 

Nae Afisa Utumishi wa Kiwanda hicho, Ahmed Mstapha amesema kuwa kiwanda cha Nyati Cement kinatekeleza majukumu yake kwa jamii inayozunguka kiwanda hicho. 

Amesema kuwa wataendelea kuwa karibu na wananchi katika shughuli mbalimbali ambazo zinajitokeza katika eneo la Kimbiji.

Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigamboni, Stephen Katemba akizungumza na wafanyakazi mara baada kutembelea kiwanda hicho katika siku ya wafanyakazi na kushiriki shughuli mbalimbali ikwemo ya upandaji jijini Dar es Salaam.
Makamu wa Rais wa Lake Cement, Afroz Ansary akizungumza juu ya udhamini wa shughuli mbalimbali zinazofanywa na kiwanda hicho.
Meneja Rasilimali Watu wa Lake Cement, Julieth Domel akizungumza juu jinsi wanavyoshugulika na wafanyakazi wa kiwanda kwa kufuata sheria za Kazi. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...