Na  Bashir  Yakub.           

Jirani  yako  au  mtu  mwingine  yeyote  amejenga   na  kuziba  njia. Njia  yoyote iwe  kubwa  kama  barabara  ama  ndogo  ambayo  hata  gari  haiwezi  kupita. Iwe  tu kama  ya   pikipiki  au  baiskeli au hata  ya  miguu  tu.  Yote  haya  hayajalishi  na hizi  zote  ni  njia kwa  mujibu  wa  sheria.

1.HAKI  YA  NJIA  KISHERIA .
Kifungu  cha  151  cha  sheria  namba  4  sheria  ya  ardhi  ya  mwaka  1999 kinaeleza  haki  hii. Kinaitambua  haki  hii  kwa  kusema  kuwa  haki  ya  njia  ipo  kwa  njia  zile  ambazo  ni  kwa ajili  ya  matumizi  ya  umma.  Umma  hapa  humaanisha  watu  wote  lakini  pia  wakazi  wa  eneo  fulani  wanaotumia  njia  hiyo  kwa  ajili  ya  shughuli  zao  mbalimbali.
Kifungu  kimepanua matumizi  ya  njia  ya  umma  kwa   kumaanisha  hata  njia  zilizotengwa  kwa ajili  ya  makampuni  binafsi. 

Kwa  mfano  kuna  sehemu  ukipita  utaona njia  au  sehemu  ya  lami  ya  barabara imekatwa  maalum  kwa  ajli  ya  kuruhusu watu  au magari  ya  kampuni  fulani  kupata  sehemu  ya  kuingilia.

Lakini  pia  zipo  njia  zimetengwa  kwa  ajili  ya  shughuli  za serikali. Haraka  utaona  kuwa haki  ya njia  haijagusa tu  kule  mitaani  wanakoishi  watu  tu  bali  hata  sehemu  za  makampuni  binafsi  nk.

2.   KUZIBA  NJIA  YA  UMMA.

Kuziba  njia  ya  umma  ni  kosa  kwa  mujibu  wa  kifungu  cha  177( 4 )  cha  sheria  ya  ardhi. Wako  watu  wakorofi  huko  mitaani  huziba  njia  kwa  makusudi.  Yawezekana kabisa  mtu  akiwa  anajua kabisa eneo  fulani  ni  njia  na  watu  hupita  hapo  lakini  kwa makusudi  au bila  kujali  akajenga  ukuta au akaweka uzio  wa  sinyenge  au  akapanda  mti  pale  au  akaweka  kifusi au  kwa  namna  nyingine  yoyote. 

Na  wengine  huambiwa  na  watu  lakini  wasisikie   kwasababu  ya  pesa,  au  urafiki  na  viongozi  wa  serikali  au  cheo  au  rushwa  au  vinginevyo.  Basi  yatupasa  kujua kuwa  watu  hawa  huwa  wakitenda  makosa  na si  wakunyamazia.

Njia  kuzibwa si  lazima  iwe  imezibwa yote.  Hata kuibana na kuitoa  katika  uhalisia  wake  katika  kiwango  chochote  nako  ni  kuziba  njia.  Njia  yafaa  iachwe  vilevile  ilivyo.
          
  KUSOMA  ZAIDI sheriayakub.blogspot.com


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...