Hatimaye utata uliokuwa umeenea wa kuwepo kwa ufujaji na matumizi mabaya ya fedha kiasi cha milioni 285.49 zilizokuwa zimechangwa na wadau pamoja na serikali kwa ajili ya rambi rambi ya vifo vya ajali ya basi la wanafunzi wa shule ya Lucky Vicent umekwisha baada ya mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo kukabidhi milioni 23.27 kwa wazazi wa watoto walionusurika katika ajali hiyo.

Akikabidhi fedha hizo mbele ya waandishi wa habari ambapo kila mzazi amepata Milioni 7.75, Bw. Gambo amesema fedha hizo zilikuwa zimebaki baada ya matumizi ya shughuli za mazishi kwa watoto 32 walimu wawili na dereva waliokuwa wamekufa katika ajali hiyo na matumizi mengine yakiwemo ya wazazi waliokuwa nchini marekani kwa ajili ya kuwauguza watoto wao na kwamba matumizi ya fedha hizo watapanga wao wenyewe.

Katika hatua nyingine Bw Gambo alisema Serikali imekubali kutoa wataam wa saikolojia kwa ajili ya kuendelea kuwasaidia watoto walionusurika katika ajali ya basi la wanafunzi ili kuwaweka sawa na pia kuwaandaa kufanya mtihani wa darasa la saba unaowakabili mnamo mwezi Septemba.

Aidha Bw, Gambo amesema kazi ya kutoa tiba ya kisaikolojia pia ilishafanyika kwa wanafunzi wa shule ya Lucky Vicent .Wakizungumza baada ya kukabidhiwa Fedha hizo wazazi wa watoto hao wameishukuru serikali na wafadhili kutoka marekani kwa msaada mkubwa kwa watoto wao tangu mwanzo hadi sasa.

Aidha wazazi hao wamesema pamoja na watoto wao kuwa nje ya shule kwa zaidi ya miezi mitatu wako tayari kufanya mtihani na kumaliza ELIMU ya msingi unaotarajiwa kufanyika mwezi September.

Kwa mujibu wa Bw Gambo baada ya kutokea kwa AJALI hiyo MWEZI May 2017 wadau MBALIMBALI na serikali walijitolea na kuchanga fedha na kupatikana zaidi ya milioni 285.49 ambazo nbaada ya matumizi zilibaki milioni 23.27 ambazo zimekabidhiwa leo.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

RC Gambo akiwakabidhi wazazi wa Doreen Mshana jumla ya Shilingi Milioni 7.75 ikiwa ni bakaa ya michango ya rambirambi.
RC Gambo akiwakabidhi wazazi wa Wilson Tarimo jumla ya Shilingi Milioni 7.75 ikiwa ni bakaa ya michango ya rambirambi.
RC Gambo akimkabidhi mzazi wa Shadhia jumla ya Shilingi Milioni 7.75 ikiwa ni bakaa ya michango ya rambirambi
Kushoto ni mtoto Shadhia na Kulia ni mtoto Wilson wakitoka nje ya jengo la ofisi ya Mkuu wa mkoa
Mhe Gambo akisalimiana na mtoto Doreen Mshana

Mhe Gambo katika picha ya pamoja na manusura wa ajali ya Lucky Vincent walipotembelea ofisi yake mapema hii leo. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...