Na Karama Kenyunko, Globu ya jamii.

Mahakama ya hakimu mkazi Kisutu, imesema uamuzi wa kupokelewa au kutokupokelewa kwa bangi iliyokutwa nyumbani kwa miss Tanzania 2006, Wema Sepetu na wenzake wawili utatolewa Septemba 12.

Hakimu Mkazi Wa Mahakama ya Hakimu Mkazi, Thomas Simba amesema hayo leo wakati kesi hiyo imekuja kwa ajili ya kutolewa uamuzi.

Katika kesi hiyo, Wema ambaye pia ni msanii maarufu wa filamu anakabiliwa na mashtaka ya kukutwa na kete mbili za bangi na msokoto mmoja pamoja na wafanyakazi wake wawili, Angelina Msigwa na Matrida Abbas.

Akiahirisha kesi hiyo, hakimu Simba amesema, " nilitakiwa kutoa uamuzi mdogo leo kuhusiana na kielelezo kilichowasilishwa na shahidi wa upande wa mashtaka kama kipokelewe au la, lakini palitakiwa kufanya utafiti wa kutosha kutolea maamuzi, nilijipa muda mdogo sana, tumejadiliana na mawakili wa pande zote mbili na sasa uamuzi utatolewa Septemba 12 na kesi hii itaendelwa hadi  Septemba 13.

Awali ilidaiwa, February mwaka huu, katika makazi ya Wema, Kunduchi Ununio washtakiwa walikutwa na msokoto mmoja na vipisi viwili vya bangi vyenye uzito Wa gramu 1.08

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...