Kitengo cha Usajili wa Hati na Nyaraka katika Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kimefanya maboresho katika upatikanaji wa Hati na Nyaraka kwa muda mfupi zaidi na ilivyokuwa hapo awali.

Akizungumza wizarani hivi karibuni; Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Hati; Bwn. Kastor Ngonyani alisema; Katika zoezi la usajili wa Hati mpya zilizokuwa zikiandaliwa kwa muda wa miezi mitatu toka tarehe ya kuwasilishwa kwa Msajili, sasa zoezi hilo linachukua wiki mbili tu. Ameeleza utaratibu huo umerahisishwa kwa kutumia mfumo wa Kielektroniki.

Aidha, Bwn. Ngonyani alisema kwa nyaraka nyingine zinazohusu Ardhi, kama zile za Uhamisho, Mikopo na zile zisizohusu Ardhi/za mali zinazohamishika zinatumia wiki moja tu kuwa tayari kutoka tarehe ambapo nyaraka husika iliwasilishwa kwa Msajili wa Hati.

Vile vile, Msajili alisema kwamba utoaji wa taarifa nyingine za upekuzi/ Search ambazo huhusisha taarifa mbalimbali kama vile; Kujua kiwanja ni cha matumizi gani, kina Hati au hakina, Mmiliki wake ni nani na taarifa zinazofanana na hizo kuhusu Historia ya kiwanja husika; " Sasa taarifa hizo zinapatikana kwa siku mbili tu, tofauti na ilivyokuwa awali ambapo zoezi hilo lilikuwa linachukua wiki mbili, mwezi mzima au hata zaidi," alisema Bwn. Ngonyani.

Bwn. Ngonyani alieleza jinsi ambavyo ofisi yake imekuwa na Hati na nyaraka mbalimbali za Wananchi ambao bado hawajafika kuchukua Hati na Nyaraka hizo, licha ya nyaraka hizo kuwa tayari kwa muda mrefu uliopita. Bwn. Ngonyani alitoa rai kwa Wananchi wote ambao walishafika katika ofisi yake kwa ajili ya kupatiwa huduma hizo wafike kuchukua Hati na Nyaraka hizo muhimu kwao.

Ofisi ya Kitengo cha Msajili wa Hati ipo kisheria . Sheria zinazoainisha uwepo wake sambamba na majukumu yake ni ; Sheria ya Usajili wa Ardhi , Sura ya 334 ya Sheria za Nchi; Sheria ya Usajili wa Nyaraka, Sura 117 ya Sheria za Nchi; Sheria ya Uhamisho wa Mali/Usajili wa Mali zinazohamishika, Sura 210 ya Sheria za Nchi na Sheria za Usajili wa Majengo ( Unit Tittle Act).

Na kitengo cha Mawasiliano Serikalini -Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi .

Msajili wa Kitengo cha Hati; Bwn. Kastor Ngonyani akizungumzia Maboresho yaliyofanyika katika ofisi yake.

Afisa katika Kitengo cha Hati akimhudumia mteja aliyefika katika dawati lake.

Maafisa mbalimbali katika Kitengo cha Hati. Na wengine wa Idara mbalimbali za Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi wakiendelea kuhudumia Wananchi katika Kituo cha Huduma kwa Mteja Wizarani hapo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...